Ng'ombe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bos)
Ng'ombe
Kundi la ng'ombe
Kundi la ng'ombe
Uainishaji wa kisayansi
Domeni: https://sw.wikipedia.org/wiki/Ng%27ombe#/media/File:Nguni_cattle.jpg
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Artiodactyla (Wanyama wenye vidole viwili au vinne mguuni)
Nusuoda: Ruminantia (Wanyama wanaocheua)
Familia: Bovidae (Wanyama walio na mnasaba na ng'ombe)
J. E. Gray, 1821
Nusufamilia: Bovinae (Wanyama wanaofanana na ng'ombe)
Jenasi: Bos (Ng'ombe)
Linnaeus, 1758
Spishi: B. primigenius
(Bojanus, 1827)
Ngazi za chini

Nususpishi 5:

B. p. africanus (Thomas, 1881)
B. p. indicus (Linnaeus, 1758)
B. p. namadicus (Falconer, 1859)
B. p. primigenius Bojanus, 1827
B. p. taurus (Linnaeus, 1758)

Kwa kundinyota inayoweza kuitwa Ng'ombe angalia hapa Tauri (kundinyota)

Ng'ombe (zamani pia bakari) ni wanyama wakubwa wanaokula nyasi. Ni wanyama wanaofugwa kwa wingi sana kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi au pia kwa kuvuta plau au gari la kukokotwa.

Kibiolojia ni wanyama wa jenasi Bos. “Ng'ombe-kaya” ni aina zifugwazo za “ng'ombe-mwitu” (Bos primigenius).

Kwa asili kuna aina mbili za ng'ombe-kaya: ng'ombe wa Ulaya na ng'ombe wa Uhindi ambazo ni nususpishi za B. primigenius (B. p. taurus na B. p. indicus mtawalia, ingawa mara nyingi nususpishi hizo zinaainishwa kama spishi za B. taurus na B. indicus). Zinatoka kwa nususpishi za zamani B. p. primigenius na B. p. namadicus.

Siku hizi ni vigumu kufahamu nususpishi za ng'ombe, kwa sababu takriban aina zote za ng'ombe ni chotara sasa.

Ng'ombe hula nyasi na hutembea kwa kwato. Ng'ombe waliofugwa na binadamu walitokana na ng'ombe-mwitu ili kujipatia nyama na maziwa. Katika nchi nyingi hutumiwa pia kama mnyama wa mizigo anayevuta plau au magari.

Wataalamu huamini ya kwamba aina zote za ng'ombe zina asili katika Mashariki ya Kati mnamo milenia ya 9 KK ambako watu waliwahi kuwafuga na kutoka hapa ufugaji ng'ombe ulisambaa kote duniani.

Ng'ombe wanapatikana kote duniani na kuna aina kwa kila namna ya hali ya hewa. Wengine huishi katika milima baridi ya Uskoti na Skandinavia, wengine katika joto la Afrika au Australia.

Wanacheua chakula chao na huwa na tumbo lenye vyumba vinne. Baada ya kula nyasi mara ya kwanza wanairudisha kutoka chumba cha kwanza cha tumbo na kuitafuna tena. Kwa njia hii wanapata lishe nyingi kutoka nyasi.

Nususpishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ng'ombe kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.