Mbuzi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ovis)

Kwa nyota zenye kutumia jina hili angalia Mbuzi (kundinyota)

Mbuzi
Mbuzi-mwitu (Capra aegagrus)
Mbuzi-mwitu
(Capra aegagrus)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Artiodactyla (Wanyama wenye vidole viwili au vinne mguuni)
Nusuoda: Ruminantia (Wanyama wanaocheua)
Familia: Bovidae (Wanyama walio na mnasaba na ng'ombe)
J. E. Gray, 1821
Nusufamilia: Caprinae
Ngazi za chini

Jenasi 13:

Mbuzi ni wanyama wakubwa kiasi wa nusufamilia Caprinae katika familia Bovidae.

Spishi kadhaa huitwa kondoo lakini kwa kiuainisho hakuna tofauti kuu kati ya makundi haya.

Spishi zote za porini zina pembe kichwani, madume na majike, lakini kuna aina za mbuzi-kaya na kondoo-kaya ambazo hazina pembe.

Spishi za mbuzi zinaweza kugawanywa katika aina mbili zenye mienendo tofauti. Spishi za aina moja huishi kwa makundi madogo na hulinda eneo dogo kiasi lenye chakula kingi dhidi ya wana wa spishi zao zenyewe. Spishi hizi zina pembe kali. Spishi za aina nyingine huishi kwa makundi makubwa katika maeneo makubwa yenye chakula kichache au cha sifa duni. Spishi hizi huwekea eneo lao alama kutoka matezi ya harufu.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Jenasi za kabla ya historia[1][2][hariri | hariri chanzo]

  • Benicerus
  • Boopsis
  • Bootherium
  • Capraoryx
  • Caprotragoides
  • Criotherium
  • Damalavus
  • Euceratherium
  • Gallogoral
  • Lyrocerus
  • Myotragus
  • Makapania
  • Megalovis
  • Mesembriacerus
  • Neotragocerus
  • Nesogoral
  • Norbertia
  • Numidocapra
  • Oioceros
  • Olonbulukia
  • Pachygazella
  • Pachytragus
  • Palaeoreas
  • Palaeoryx
  • Paraprotoryx
  • Parapseudotragus
  • Parurmiatherium
  • Praeovibos
  • Procamptoceras
  • Prosinotragus
  • Protoryx
  • Pseudotragus
  • Samotragus
  • Sinocapra
  • Sinomegoceros
  • Sinopalaeoceros
  • Sinotragus
  • Sivacapra
  • Soergelia
  • Sporadotragus
  • Symbos
  • Tethytragus
  • Tossunnoria
  • Tsaidamotherium
  • Turcocerus
  • Urmiatherium

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.