Watoto wa Bethlehemu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro mdogo wa karne ya 10.
Maangamizi ya Wasio na Hatia (sehemu) kadiri ya Lucas Cranach the Elder (1515 hivi), National Museum huko Warsaw, Polandi.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Watoto wa Bethlehemu (waliuawa 5 KK hivi) ni watoto wa kiume wa chini ya miaka 2 waliopatikana Bethlehemu na kuuawa kwa agizo la mfalme Herode Mkuu (Math 2:16-18).

Sababu ni kwamba mamajusi kutoka mashariki walikuwa wamefika Yerusalemu ili kumtafuta mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa na hatimaye kumzawadia. Habari hiyo ilimshtusha Herode na kumfanya atake kumuua.

Aliposikia kwamba mamajusi walirudi kwao kutoka Bethlehemu bila kumpa taarifa kamili juu ya mtoto, aliagiza wauawe watoto wote wa kiume wa kijiji hicho wenye umri chini ya miaka 2.[1]

Imekadiriwa kwamba watoto hao waliweza kuwa 20-40 hivi[2][3].

Hata hivyo, mlengwa mwenyewe, Yesu, alinusurika kwa wazee wake kutoroka naye hadi Misri, waliposhi kama wakimbizi mpaka baada ya kifo cha Herode.

Kwa kuwa watoto hao waliuawa kwa niaba ya Yesu, wanaheshimiwa na Wakristo wa madhehebu mengi kama wafiadini[4].

Sikukuu yao inaadhimishwa tangu karne ya 5, hasa tarehe 27 Desemba na 28 Desemba[5].

Ingawa habari hiyo haipatikani nje ya Injili, tabia ya Herode ilikuwa ya namna hiyo, hata aliua watoto wake 3, mke wake mmojawapo na mama-mkwe[6][7].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Matthew 2:17: "Then was fulfilled that which was spoken through Jeremiah the prophet, saying, 'A voice is heard in Ramah, mourning and great weeping, Rachel weeping for her children and refusing to be comforted, because her children are no more.'"
  2. Raymond E. Brown
  3. Donald A. Hagner, World Biblical Commentary, Matthew 1-13, page 37
  4. Bill Doggett, Gordon W. Lathrop, New Proclamation Commentary on Feasts, Holy Days, and Other Celebrations, (Fortress Press, 2007) page 43.
  5. Martyrologium Romanum
  6. Josephus, Antiquities of the Jews, Book XV (at Wikisource)
  7. R. T. France, addressing the story's absence in Antiquities of the Jews, argues that "the murder of a few infants in a small village [is] not on a scale to match the more spectacular assassinations recorded by Josephus". R. T. France, "The Gospel of Matthew", NICNT (2007)

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Albright, W. F. and C. S. Mann. "Matthew." The Anchor Bible Series. New York: Doubleday & Company, 1971.
  • Clarke, Howard W. The Gospel of Matthew and its Readers: A Historical Introduction to the First Gospel. Bloomington: Indiana University Press, 2003.
  • Robert Eisenman, 1997. James the Brother of Jesus: The Key to Unlocking the Secrets of Early Christianity and the Dead Sea Scrolls. Viking/Penguin.
  • Goulder, M. D. Midrash and Lection in Matthew. London: SPCK, 1974.
  • Jones, Alexander. The Gospel According to St. Matthew. London: Geoffrey Chapman, 1965.
  • Schweizer, Eduard. The Good News According to Matthew. Atlanta: John Knox Press, 1975.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Watoto wa Bethlehemu kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.