Kitabu cha Methali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kitabu cha Methali kwa Kiebrania.

Kitabu cha Mithali kimo katika Tanakh (Biblia ya Kiebrania), hivyo pia katika Agano la Kale la Biblia ya Kikristo ambamo ni cha kwanza kati ya vitabu vya hekima.

Historia yake[hariri | hariri chanzo]

Kweli kitabu hicho kinaonekana cha zamani kuliko vile vya hekima vinavyofuata; labda kilikamilika katika karne ya 4 KK, kisha kukusanya tafakuri za vizazi kadhaa juu ya maisha kwa mtazamo wa kibinadamu na wa imani.

Lugha yake[hariri | hariri chanzo]

Kitabu kiliandikwa kwa Kiebrania na kutafsiriwa kwa mara ya kwanza katika lugha ya Kigiriki huko Misri (tafsiri maarufu kama Septuaginta).

Yaliyomo[hariri | hariri chanzo]

Yaliyomo ni maadili ambayo yamuongoze mtu maishani ili awe na heri.

Ufafanuzi wake[hariri | hariri chanzo]

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu cha Methali kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.