Tanakh
Mandhari

Tanakh (kwa Kiebrania: תנ״ך) ni jina la Biblia ya Kiebrania kwa lugha asili. Tanakh ni kifupi kinachounganisha herufi tatu "T" - "N" - "Kh" ambazo ni za kwanza katika maneno matatu ya Kiebrania yanayotaja sehemu tatu zinazounda Biblia hiyo.
- 1. Torah (תורה) ni Torati au vitabu vitano vya kwanza vinavyoitwa pia "vitabu vya Musa". Mara nyingi vyaitwa pia "sheria" katika imani ya Uyahudi. Hivi ni vitabu vinavyoitwa ama Kitabu cha kwanza, cha pili, cha tatu n.k. cha Musa au kwa majina yafuatayo:
- Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati.
- Majina ya Kiebrania ya vitabu hivyo ni maneno ya kwanza ya Kiebrania ya kila kitabu: Bereshit (בְּרֵאשִית) yaani "mwanzo" (Hapo mwanzo..); Shemot (שְמוֹת) yaani "majina" (Basi majina ya wana wa Israeli...); Wayikra (וַיִּקְרָא) yaani "akaita" (Bwana akamwita Musa...); Bemidbar (בְּמִּדְבַּר) yaani "nyikani" (Bwana akanena na Musa katika nyika ya Sinai...); Devarim (דְּבָרִים) yaani "maneno" (Haya ndiyo maneno...).
- Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati.
- 2. Nevi'im (נביאים) ni manabii yaani maandiko ya maneno na matendo ya manabii katika Uyahudi. Humo huhesabiwa vitabu kama
- 3. Ketuvim (כתובים) ni "maandiko" (Kiebrania "ketuv" ni sawa na Kiarabu/ Kiswahili "kitab/kitabu"). Vitabu hivyo hugawanywa katika makundi ya:
- vitabu vya kihistoria kama vile Ezra, Nehemia na Mambo ya Nyakati.
- vitabu vya hekima kama vile Ayubu, Mhubiri na Mithali.
- vitabu vya kishairi kama vile Zaburi, Maombolezo na Wimbo Ulio Bora.
- vitabu vingine kama vile Ruthu, Estha na Danieli.
Mgawanyo huo wa vitabu ni tofauti kiasi na namna ya kuvipanga katika Biblia ya Kikristo vinamopatikana katika sehemu yake ya kwanza ambayo inaitwa Agano la Kale na kufuatwa na Agano Jipya lililoandikwa baada ya Yesu ambaye Wakristo wanaamini ndiye Masiya aliyetabiriwa tangu kale. Wakristo wanawauliza kaka zao Wayahudi: imekuwaje ufunuo wa Mungu kwao ulisimama tangu miaka zaidi ya 2000 ingawa wao wanamsubiri bado Masiya afike? Je, historia ya wokovu imekatika?
| Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Tanakh kama historia yake au athari wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |