Kitabu cha Baruku

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kitabu cha Baruk)

Kitabu cha Baruku ni kimojawapo kati ya vitabu vya deuterokanoni vya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Uandishi[hariri | hariri chanzo]

Kadiri ya utangulizi wake (Bar 1:1-14), kiliandikwa na Baruku, karani wa nabii Yeremia, wakati wa uhamisho wa Wayahudi huko Babuloni katika karne ya 6 K.K..

Hata hivyo wataalamu wanaona kiliandikwa katika karne ya 2 K.K. moja kwa moja katika lugha ya Kigiriki, isipokuwa labda sehemu ya pili inatokana na andiko asili la Kiebrania.

Mazingira[hariri | hariri chanzo]

Kitabu kinatuingiza katika Uyahudi wa mtawanyiko na kutuonyesha jinsi maisha maadilifu ya kidini yalivyodumishwa kwa kuhusiana na Yerusalemu, kwa kudumisha sala na kushika Torati.

Ufafanuzi[hariri | hariri chanzo]

Kama vitabu vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu cha Baruku kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.