Bad ni jina la kutaja albamu ya saba ya mwanamuziki, mtayarishaji wa rekodi, mwimbaji, mfanyabiashara, kabaila, na mhisani wa Kimarekani, Michael Jackson. Albamu ilitolewa mnamo tar. 31 Agosti1987 na studio ya Epic/CBS Records. Rekodi ya albamu hii ilitolewa karibuni miaka mitano tangu kutoka kwa albamu ya awali. Miaka ishirini baada ya kutolewa, albamu imeuza takriban nakala zaidi ya milioni 30 kwa dunia nzima, na kopi milioni 8 ziliuzwa nchi za nje kwa kupitia Marekani peke yake. Bad ni albamu ya kwanza, na ndiyo hadi sasa albamu pekee, iliyoweza kuingiza single tano katika Billboard Hot 100 zikiwa nafasi ya 1.[3]
Katika albamu hii, Jackson ameonekana kuwa huru zaidi kupita zile albamu zake za mbili za awali, Off the Wall na albamu yenye mauzo bora kwa muda wote, Thriller. Humu katunga nyimbo tisa katika kumi na moja za albamu, na amesaidia kutunga na kutayarisha wimbo wa "Man in the Mirror". Pia humu amekuja na sura mpya ya mshangao.
Albamu iliendelea kupata mafanikio makubwa katika miaka ya 1980 na imeshinda tuzo mbili za Grammy, moja kwa Muziki Bora wa Video - Leave Me Alone na nyingine kwa ajili ya Uhandisi Bora wa Albamu, Bruce Swedien na Humberto Gatica.[4] Mnamo mwaka 2009, Bad pia, imewekwa nafasi ya 43 katika orodha ya Albamu Bora 100 za Karne za MTV zilizoorodheshwa na VH1.[5] Albamu pia iliwekwa nafasi ya 202 katika orodha ya gazeti ya Rolling Stone, Albamu Bora ya Karne.[6]