Afya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Stempu ya posta ya New Zealand, mnamo mwaka 1933.
Mwanamke akinawa mikono 1655 hivi.
Donald Henderson na wenzake katika kukinga watu dhidi ya ndui mwaka 1966.

Afya ni hali ya kujisikia vizuri kimwili, kiakili, kiroho na kiutu bila kusumbuliwa na ugonjwa wowote.

Afya ya binadamu itakuwa njema kama atafuatilia kanuni na taratibu bora za afya. Hiyo inajumuisha mlo kamili, yaani chakula chenye virutubishi vyote, vikiwemo protini, wanga na mafuta (hiyo iwe katika asilimia ndogo sana).

Pia anatakiwa awe msafi mwilini na mazingira yake, kama vile kwa kuoga na kusafisha mazingira yanayomzunguka. Mandhari yenye hewa safi pia husaidia katika kuhifadhi afya ya binadamu katika mwili na akili.

Mazingira mara nyingi huchukuliwa kuwa jambo muhimu katika hali ya afya ya binadamu. Hii inajumuisha mazingira ya asili, mazingira ya kujengwa, na mazingira ya kijamii. Pia mambo kama vile maji safi na hewa, makazi salama, huchangia afya nzuri, hasa kwa afya ya watoto wachanga na watoto.[1]

Utafiti umeonyesha kuwa ukosefu wa maeneo ya burudani husabsabisha kupungua kwa afya na ustawi.[2]


Pia anatakiwa kuwa na afya ya kiroho yaani kuishi kadiri ya mafundisho ya Mwenyezi Mungu kama vile: kupendana na wengine, kuthaminiana na kuacha dhambi: mara nyingi hizo zinadhuru afya ya mwili pia.

Fafanuzi za afya[hariri | hariri chanzo]

Sawa na suala la ugonjwa, hakuna elezo kamili kuhusu hali ya afya.


  • Kwa watu wengi ni hali ya kutosumbuliwa na maumivu na udhaifu, pamoja na uwezo wa kutumia sehemu zote za mwili. Ni wazi ya kwamba hisia hii ni tofauti kati ya mtu na mtu.

Majukumu[hariri | hariri chanzo]

Serikali zinatarajiwa kuandaa wataalamu wa mambo ya afya na kujenga hospitali nyingi hata vijijini kwa sababu watu wengi hupoteza maisha kwa kukosa huduma za afya: hii itasaidia kupunguza vifo.

Watu wanatakiwa kuwa na ustadi wa kufanya mazoezi kwa wingi. Hata mjamzito anapaswa kufanya mazoezi, ingawa si kazi ngumu.

Pia kula mlo bora wakati wote ili kuepukana na magonjwa yanayotokana na ukosefu wa chakula fulani (virutubishi).

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. http://www.who.int/hia/evidence/doh/en/
  2. Faida za maeneo ya burudani kwenye afya.
  3. WHO definition of Health.
  4. Makala inayomnukuu Talcott Parsons.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Afya kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.