Mafuta (chakula)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Makorosho yana mafuta mengi mazuri

Mafuta au shahamu ni sehemu za chakula pamoja na wanga, protini na vitamini. Neno "fati" (kutoka Kiing. fat) afadhali lizuiwe. Vyakula vilivyo na mafuta mengi ni k.m. maparachichi, karanga, makorosho, mbegu kama alizeti na siagi.

parachichi
Parachichi

Vyakula hivi humsaidia mtu kwa kumpatia joto hasa wakati wa baridi, pia huchangia katika uzalishaji wa nishati na nguvu kwa ajili ya mwili na pia hufanya kazi mbalimbali katika mmeng'enyo wa chakula tumboni.

Athari za mafuta mengi mwilini[hariri | hariri chanzo]

Upande wa kushoto ni panya mwenye mafuta mengi na pembeni yake ni mwenye mafuta ya kawaida.

Vyakula hivi huhitajika kwa asilimia chache sana ndani ya mwili. Vyakula vya mafuta vikizidi mwilini huwa na madhara kama kuziba mishipa na kusababisha ugonjwa huitwao shinikizo la damu au maarufu kama presha. Ugonjwa huu hutokana na mafuta kuganda moyoni na kusababisha moyo kushindwa kusukuma damu ipasavyo.

Pamoja na hayo, huenda ukawanda kupindukia ukawa mnene mno. Hili likifanyika, wafaa ufanye mazoezi na ule chakula kisicho na ufuta mwingi. Hata hivyo kuwanda si ishara kwamba umekula sana, maana kuwa watu ambao hunenepa maana ile hali iko katika nasaba yao (hereditary genes).

Kusafisha ufuta mwilini[hariri | hariri chanzo]

Kwa watu walio na mafuta mengi mwilini, jambo la kwanza wanalohimizwa kufanya ni kusafisha ufuta mwilini kwa njia ya kuondoa sumu ("detoxing").

Ni vyema pia kufanya mazoezi kila siku

Yafaa unywe maji mengi maana maji husaidia katika metaboli

Yafaa ule chakula kisicho na ufuta kupindukia.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mafuta (chakula) kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.