Vitamini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Matunda ni chanzo muhimu cha vitamini

Vitamini ni kirutubishi kinachohitajika na mwili kwa kujenga afya yake. Kwa lugha nyingine, kampaundi ogania zilizo lazima kwa shughuli za mwili lakini haziwezi kutengenezwa na mwili wenyewe ni lazima kuzipata kupitia chakula. Viumbehai wanaweza kuishi bila matata wakikosa vitamini kwa muda mfupi lakini uhaba wa muda mrefu unaleta magonjwa.

Vitamini inaitwa mara nyingi kwa herufi kama vitamini A, vitamini B, vitamini C na kadhalika.

Vitamini hutofautiana kati ya viumbe maana kama kemikali huitwa "vitamini" inategemea kama kiumbe fulani anaweza kutengeza kemikali hiyo ndani ya mwili wake au la. Kwa mfano vitamini C ni asidi askobini na wanyama wengi wanaitengeneza ndani ya miili yao; lakini sehemu ya mamalia, hasa nyani wakubwa (primates) pamoja na binadamu, hawawezi kuitengeneza hivyo wanahitaji chakula chenye asidi hiyo ambayo hupatikana hasa kwenye matunda kama limau au chungwa.

Leo hii vitamini nyingi kwa mahitaji ya binadamu hutengenezwa viwandani na kupatikana kama vidonge.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vitamini kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.