Shirika la Afya Duniani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Shirika la Afya Duniani (kwa Kiing. World Health Organization - kifupi: WHO) ni kitengo cha Umoja wa Mataifa. Inashughulika habari za afya ya umma ikilenga kuunganisha juhudi za kitaifa za kupambana na magonjwa na kujenga afya.

Kisheria WHO ni shirika lenye madola wanachama 193.

Kati ya shughuli muhimu za WHO ni programu za kupambana na magonjwa yanayoathiri watu wengi kama vile Malaria, Ukimwi au SARS. Hata hivyo wapo wanaoilaumu kwa kuhamasisha sera nyingine, kama utoaji mimba na udhibiti wa uzazi hata bila ya wahusika kujua[1].

WHO inaratibu mipango ya kutengeneza na kusambaza dawa za kinga. Inaratibu pia miradi ya chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali[2].

Kanda za WHO

Makao makuu ya WHO yapo Geneva (Uswisi). Kuna ofisi sita za kikanda kama zifuatazo:

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  1. https://www.lifesitenews.com/news/new-documentary-exposes-world-health-organizations-vaccine-sterilization-campaign-in-kenya/
  2. https://www.lifesitenews.com/news/new-documentary-exposes-world-health-organizations-vaccine-sterilization-campaign-in-kenya/