New Delhi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Jiji la New Delhi
Jiji la New Delhi is located in Uhindi
Jiji la New Delhi
Jiji la New Delhi

Mahali pa New Delhi katika Uhindi

Majiranukta: 28°40′0″N 77°13′0″E / 28.66667°N 77.21667°E / 28.66667; 77.21667
Nchi Uhindi
Tovuti:  http://www.ndmc.gov.in/
"India Gate" mjini New Delhi.
Boma Jekundu la Delhi ni jengo mashuhuri lililojengwa kwa Shah Jahan.
Majengo ya serikali katika Delhi Mpya yalijengwa na Waingereza.

New Delhi (yaani Delhi Mpya; kwa Kihindi: |नई दिल्ली, kwa Kiurdu: نئی دلی) ni mji mkuu wa Uhindi na kitovu cha jiji kubwa la Delhi. Pamoja na Delhi yote kuna wakazi zaidi ya milioni kumi.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Iko kaskazini mwa nchi kwenye kingo za mto Yamuna katika tambarare ya bonde la Ganga. Mji huo uko m 216 juu ya UB kwa wastani.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Delhi ina historia ndefu sana iliyoanza mnamo mwaka 1200 KK. Iliharibiwa mara nyingi na kujengwa upya na kubadilisha jina pamoja na wakazi na watawala wake. Katika karne zilizopita ilikuwa mji mkuu wa Dola la Moghul na tangu mwaka 1911 wa Uhindi wa Kiingereza.

Delhi Mpya ilianzishwa baada ya azimio la George V, mfalme wa Uingereza na Kaisari wa Uhindi, la kuhamisha mji mkuu kutoka Kolkata kwenda Delhi. Mji mpya ulijengwa kando ya Delhi ya Kale na kukabidhiwa mwaka 1931. Ulisanifiwa na wasanifu Waingereza Edwin Lutyens (1869-1944) na Herbert Baker (1862-1946).

Tangu mwaka 1947 New Delhi ni mji mkuu wa Uhindi huru.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu New Delhi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.