Nenda kwa yaliyomo

Addai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Addai katika picha takatifu ya monasteri ya Mt. Katerina kwenye mlima Sinai, Misri.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho   Utoto wa Yesu   Ubatizo   Arusi ya Kana   Utume wa Yesu   Mifano ya Yesu   Miujiza ya Yesu   Kugeuka sura   Karamu ya mwisho   Msalaba wa Yesu   Maneno saba   Kifo cha Yesu   Ufufuko wa Yesu   Kupaa mbinguni   Ujio wa pili  Yesu na matabiri ya Agano la Kale   Injili   Majina ya Yesu katika Agano Jipya   Yesu kadiri ya historia   Tarehe za maisha ya Yesu   Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi   Kiaramu   Bikira Maria   Yosefu (mume wa Maria)   Familia takatifu   Ukoo wa Yesu   Ndugu wa Yesu   Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya  · Mitazamo ya Kikristo   Mitazamo ya Kiyahudi   Mitazamo ya Kiislamu   Yesu katika sanaa

Addai, kwa Kiaramu ܐܕܝ,[1] ni mtakatifu anayeheshimiwa na madhehebu mengi ya Ukristo, hasa wa Mashariki, ingawa hakuna makubaliano ya wanahistoria kuhusu maisha yake.

Masimulizi juu yake

[hariri | hariri chanzo]

Kadiri ya mapokeo, hasa ya kitabu Mafundisho ya Addai, alikuwa Myahudi mzaliwa wa Edessa, wakati ule sehemu ya Syria, siku hizi nchini Uturuki.

Alipokwenda kuhiji Yerusalemu, alimsikiliza Yohane Mbatizaji na kubatizwa naye katika mto Yordani, akabaki Palestina.

Baadaye akawa mfuasi wa Yesu, akachaguliwa naye kati ya wanafunzi 70 kwenda kuhubiri wawiliwawili.

Baada ya ufufuko wa Yesu na Pentekoste ya mwaka uleule, Addai alianza kuhubiri Injili huko Mesopotamia, Syria na Persia.

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Agosti, pamoja na mwanafunzi wake Mari.

Hata leo inatumika anafora yenye majina yao isiyo na simulizi la Karamu ya mwisho, tofauti na nyingine zote.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. Charles George Herbermann, The Catholic Encyclopedia (Universal Knowledge Foundation, 1913), p. 136.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.