Angela Merkel
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Dk. Angela Dorothea Merkel (amezaliwa tar. 17 Julai 1954, mjini Hamburg) ni mwanasiasa wa Kijerumani, na ni Chansela wa Ujerumani tangu 22 Novemba, 2005.
Alizaliwa mjini Hamburg, na alikulia katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani (ambayo ilikuwa Ujerumani ya Mashariki, kabla ya Ujerumani zote mbili kuungana na kuwa moja) ambapo aliishi huko hadi Muungano wa Ujerumani ulipofanyika mnamo mwaka wa 1990.
Merkel ameolewa na Bw. Joachim Sauer, ambaye ni profesa wa kemia. Angela Merkel kwa sasa ni mwenyekiti wa chama cha Chama cha Kikristo cha Kidemokrasia cha Ujerumani (CDU).
Merkel amekuwa mwanamke wa kwanza kuwa chansela kunako tar. 22 Novemba 2005 katika mgongano mkubwa wa vyama viwili vya kisiasa vya Kijerumani, yaani kati ya CDU/CSU na SPD.
Mwaka 2009 alitangaza ya kwamba alielekea kuaachana na SPD akitafuta ushirikiano na cha cha FDP. Uchaguzi wa bunge wa Septemba 2009 ulirudisha chama chake cha CDU tena kama chama kikubwa akaendelea kuunda serikali mpya pamoja na FDP.
|
|
|
|---|---|
| Otto von Bismarck · Leo von Caprivi · Prince Chlodwig zu Hohenlohe-Schillingsfürst · Bernhard von Bülow · Theobald von Bethmann Hollweg · Georg Michaelis · Georg von Hertling · Prince Maximilian of Baden | |
| Kipindi cha Mapinduzi (1918–1919) | Friedrich Ebert |
| Philipp Scheidemann · Gustav Bauer · Hermann Müller · Konstantin Fehrenbach · Joseph Wirth · Wilhelm Cuno · Gustav Stresemann · Wilhelm Marx · Hans Luther · Wilhelm Marx · Hermann Müller · Heinrich Brüning · Franz von Papen · Kurt von Schleicher | |
| Adolf Hitler · Joseph Goebbels · Lutz Graf Schwerin von Krosigk | |
| Konrad Adenauer · Ludwig Erhard · Kurt Georg Kiesinger · Willy Brandt ·Walter Scheel mtendaji · Helmut Schmidt · Helmut Kohl · Gerhard Schröder · Angela Merkel | |
| Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Angela Merkel kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |