Nishati mbadala
Nishati mbadala ni aina za nishati kutoka vyanzo asilia kama vile mwanga wa jua, nguvu ya upepo, mvua, joto kutoka ardhi, mwendo wa kupwakujaa, kuni au aina nyingine za biomasi na mengine. Kwa jumla ni vyanzo vya nishati visivyokwisha kutokana na matumizi au kupoa haraka.
Tofauti yake ni fueli za kisukuku ambazo zinatoka kwenye vyanzo kama makaa mawe, gesi asilia au mafuta ya petroli zinazoendelea kupungua kadri zinazotumiwa.
Yaliyomo |
Matumizi ya nishati mbadala [hariri]
Mwaka 2008 takriban 19 - 20% ya matumizi ya nishati duniani yametokea kwenye nishati mbadala; sehemu kubwa ya takriban 13% kutoka biomasi hasa kuni na 3.2 % kutoka nguvu ya umememaji. Vyanzo vipya kama umeme kutoka upepo, umeme wa nishatijua, joto kutoka ardhini na umeme kutoka mwendo wa kupwakujaa vilileta asilimia 3 pekee lakini kiwango hiki kinazidi kuongezeka haraka. [1]
Hali halisi manufaa kutoka nishati ya jua ni kubwa zaidi sana kwa sababu matumizi yote ya mimea, mazao na matunda yana nishati ya jua kama msingi wake; pia kiwango cha joto la mazingira kinasababishwa na jua lakini katika takwimu hizi zintaja viwango tu vinavotumiwa na jitihada za kibinadamu kubadilisha mazingira asilia kama kupasha moto manyumbani, kupika vyakula, uzalishaji umeme, kuendesha usafiri na kadhalika.
Katika uzalishaji wa umeme duniani asilimia ya nguvu ya umememaji ilkuwa takriban 15%.
Kuongezeka kwa nguvu ya upepo [hariri]
Teknolojia ya kuzalisha umeme kwa nguvu ya upepo imepanuka sana katika miaka iliyopita. Mwisho wa mwaka 2009 ujazifu wa umeme kutoka chanzo hiki kilikuwa megawati 157,900 ambazo ni ongezeko la 31 % tangu mwanzo wa mwaka uleule. [2]
Maendeleo haya yalitokea mwanzoni katika Ulaya hasa Ujerumani, Denmark na Uingereza lakini miaka ya nyuma Marekani na China zlongeza pia jitihada zao kupanusha chanzo hiki cha umeme. [3][4]
Katika nchi ya Denmark umeme kutoka nguvu ya upepo ni tayari asilimia 19 ya matumizi yote ya kitaifa. [5]
[hariri]
Seli za umemenuru zinabadilisha mwanga wa jua kuwa umeme. Teknolojia hii inaendelea haraka sana na gharama za seli hizi zimeshuka. Kuna vituo vingi hasa Ulaya ambako serikali zimetoa misaada kwa kutegeneza vituo hivi na matumizi ya teknolojia hii. [6]
Meisho wa mwaka 2010 vituo vikubwa duniani zilikuwa :
- Sarnia Photovoltaic Power Plant (Canada, 97 MW),
- Montalto di Castro Photovoltaic Power Station (Italy, 84.2 MW)
- Finsterwalde Solar Park (Germany, 80.7 MW),
- Rovigo Photovoltaic Power Plant (Italy, 70 MW),
- Olmedilla Photovoltaic Park (Spain, 60 MW),
- Strasskirchen Solar Park (Germany, 54 MW)
- Lieberose Photovoltaic Park (Germany, 53 MW).
Vituo vikubwa zaidi hutengenezwa.[7]
Maejeo [hariri]
- ↑ REN21 (2010). Renewables 2010 Global Status Report p. 15-16.
- ↑ Lars Kroldrup. Gains in Global Wind Capacity Reported Green Inc., 15 Februari 2010.
- ↑ Global wind energy markets continue to boom – 2006 another record year (PDF).
- ↑ Global Wind Energy Council (2009). Global Wind 2008 Report, p. 9, accessed on 4 Januari 2010.
- ↑ International Energy Agency (2009). IEA Wind Energy: Annual Report 2008 p. 9.
- ↑ Denis Lenardic. Large-scale photovoltaic power plants ranking 1 - 50 PVresources.com, 2010.
- ↑ Mark Z. Jacobson (2009). Review of Solutions to Global Warming, Air Pollution, and Energy Security p. 4.
Viungo vya Nje [hariri]
| Wikinews has related news: EU adopts renewable energy measures |