Mombasa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sehemu za Mji wa Mombasa






Mombasa

Bendera

Nembo
Mombasa is located in Kenya
Mombasa
Mombasa

Mahali pa mji wa Mombasa katika Kenya

Majiranukta: 4°03′S 39°40′E / 4.050°S 39.667°E / -4.050; 39.667
Nchi Bendera ya Kenya Kenya
Kaunti Mombasa
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 1,200,000
Mombasa.

Mombasa ni mji mkubwa wa pili wa Kenya na wenye bandari muhimu zaidi Afrika Mashariki. Mji huu uko kwenye mwambao wa Bahari Hindi.

Baada ya kuundwa kwa serikali ya ugatuzi, Mombasa umekuwa mji mkuu wa kaunti ya Mombasa.

Mombasa ni kitovu cha utalii wa pwani ya Kenya. Watalii wengi hufika kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Moi. Wengine pia husafiri kupitia barabara kutoka Nairobi wakitazama mandhari mbalimbali. Kutoka Nairobi kwenda Mombasa ni takribani kilomita 483.77. Watalii wengi hupenda kuuona mji wa Mombasa kwanza, kisha wanaunganisha ndege hadi Kilimanjaro na sehemu nyingine zilizo na vivutio nchini Tanzania.

Kati ya ishara ya mji ni Boma la Yesu na pembe za Mombasa.

Mnamo mwaka wa 2016, mji wa Mombasa ulikuwa na idadi ya wakazi takriban milioni moja nukta mbili kwenye kisiwa cha Mombasa pamoja na sehemu zake barani. Wengi wao ni Waislamu.

Kiswahili cha Mombasa huitwa Kimvita.

Mombasa na Seattle ni "miji-ndugu".

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: