Mombasa
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mombasa ni mji mkubwa wa pili wa Kenya mwenye bandari muhimu zaidi ya Afrika Mashariki. Iko kwenye mwambao wa Bahari Hindi. Kuna wakazi 900,000 kwenye kisiwa cha Mombasa pamoja na sehemu zake barani.
Mombasa ni kitovu cha utalii wa pwani la Kenya. Watalii walio wengi hufika kweye kiwanja cha ndege cha Moi.
Kiswahili cha Mombasa chaitwa "Kimvita".
Mombasa na Seattle ni "miji-ndugu".
| Makala hiyo kuhusu "Mombasa" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Mombasa kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |

