Meru, Kenya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Meru, Kenya


Meru
Meru is located in Kenya
Meru
Meru

Mahali pa mji wa Meru katika Kenya

Majiranukta: 0°3′0″N 37°39′0″E / 0.05000°N 37.65000°E / 0.05000; 37.65000
Nchi Kenya
Kaunti Meru
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 240,900
Tovuti:  www.merutown.com

Meru ni mji wa Kenya mashariki ambao ni makao makuu ya Kaunti ya Meru na mji wa nane kwa ukubwa nchini Kenya.

Meru imeunda baraza la manispaa lenye wakazi 240,900[1].

Meru iko pande za Mto Kathita, katika mteremko wa kaskazini mashariki wa Mlima Kenya.

Mji huu uko umbali wa maili tano kaskazini mwa ikweta, urefu wa futi 5000, katika eneo la mchanganyiko wa misitu mahali wazi, miji midogo, vijiji, mashamba vijijini na wengi wa wakazi ni wa Ameru.

Unaweza kufikia mji huu ukitumia barabara ya lami, kwa vyovyote vile kama kutoka kusini kuzunguka upande wa mashariki wa Mlima Kenya, kupitia Embu, au kutoka katika eneo la kaskazini magharibi kuzunguka magharibi na kaskazini wa Mlima Kenya, kupitia Nanyuki na Timau.

Kaunti ya Meru ni mahali pa kuzuru Ili kutembelea eneo za kuhifahia wanyama ambazo ni Samburu na Buffalo Springs Lewa Downs, ambazo ziko mbali kiasi kaskazini mwa Meru, pamoja na Samburu na Buffalo Springs kupitia Isiolo, na Hifadhi ya Taifa ya Meru, katika kaskazini mwa Meru, kupitia Maua katika vilima vya Nyambeni.

Meru ni mji wa biashara, kilimo na elimu kaskazini ymw Kenya. Mji huu una mabenki na hoteli, masoko na vituo vya usafirishaji. Kahawa, chai, mbao, ng'ombe, maziwa, maharagwe ya "Kifaransa" na bidhaa nyingine nyingi hutoka katika Kaunti ya Meru. Pia kuna shule za msingi na sekondari, zikiwa pamoja na Shule kuu ya sekondari ya Meru na shule ya wasichana ya kaaga, ambazo ni baadhi ya chuo zinazoongoza katika taasisi za elimu ya sekondari Kenya. Chuo kikuu cha Emory ina ubia na Shule kuu ya sekondari ya Meru katika kusidiana na kompyuta, vitabu, na vifaa vya sayansi katika kumbukumbu ya George Brumley. Pia kuna shule za Ufundi. Taasisi ya ufundi Meru na Chuo cha Teknolojia ya Meru ambazo ndizo kuu. Pia, kuna vyuo vya ualimu na chuo kikuu cha Kenya Methodist University kinachojulikana kama KEMU.

Ni eneo muhimu la uzalizaji wa kahawa. inakuzwa na wengi wa wakulima wadogo, nakukuzwa chini ya kivuli. Mazao ya kahawa katika eneo la Meru huja mara mbili kwa mwaka, sawa n misimu miwili ya mvua, lakini mazao kuu katika Meru inakuja katika wakati tofauti kwa kiasi fulani kuliko mahali pengine nchini Kenya, kutokana na tofauti ya hali ya hewa kwenye kaskazini wa miteremko ya mlima Kenya na vilima vya Nyambenene. pia hukuzwa katika miinuko iliyo juu katika mchanga wa volkeno katika wilaya hii. Kahawa hii inatayarishwa na vyama vya ushirika vya wakulima wa kahawa ambavyo ni wenyewe viwanda vilivyo karibu na wakulima.

Meru ndio eneo kuu la ukuzaji wa Miraa (Khat) nchini Kenya. Wakulima wengi wanapendelea kuzalisha miraa kwa kuwa ina faida kubwa kifedha.

Makumbusho ya Taifa ya Meru yako katika mji.

Orodha ya Wameru maarufu[hariri | hariri chanzo]

Orodha ya hoteli katika Meru[hariri | hariri chanzo]

  • Hotel Incredible
  • Blue towers Hotel
  • White Star Hotel
  • Three steers hotel
  • Meru County Hotel
  • Meru Safari Hotel
  • Hotel ya Royal Prince
  • Simba Wells
  • Timau River Lodge

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.

Coordinates: 0°03′N 37°39′E / 0.050°N 37.650°E / 0.050; 37.650