Bungoma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bungoma


Bungoma
Bungoma is located in Kenya
Bungoma
Bungoma

Mahali pa mji wa Bungoma katika Kenya

Majiranukta: 0°34′0″N 34°34′0″E / 0.56667°N 34.56667°E / 0.56667; 34.56667
Nchi Kenya
Kaunti Bungoma
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 81,151

Bungoma ni mji wa Kenya ya magharibi karibu na mpaka wa Uganda ambao ni makao makuu ya kaunti ya Bungoma.

Wakazi walikuwa 81,151 wakati wa sensa ya mwaka 2009[1].

Bungoma iko kwenye kimo cha mita 1,385 juu ya UB, mguuni pa Mlima Elgon.

Wenyeji wa Bungoma ni Wabukusu ambao ni tawi la Waluhya.

Mji wa Bungoma ulianzishwa kama kituo cha reli ya Uganda katika miaka ya 1920. Bungoma ikateuliwa kama kituo cha mwisho ndani ya Kenya kabla ya kufikia mpaka wa Uganda.

Wakati wa uhuru Bungoma ilionekana kama kijiji kikubwa chenye maduka machache. Mji ukaendelea kukua haraka.

Uchumi umetegemea hasa kilimo kinachostawi vizuri kutokana na hali ya hewa na wingi wa mvua. Kuna kiwanda cha sukari. Kiwanda cha karatasi cha Webuye kipo karibu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.