Kitale

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kitale, Kenya


Kitale
Kitale is located in Kenya
Kitale
Kitale

Mahali pa mji wa Kitale katika Kenya

Majiranukta: 1°01′0″N 35°0′0″E / 1.01667°N 35.00000°E / 1.01667; 35.00000
Nchi Kenya
Kaunti Trans-Nzoia
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 106,187

Kitale ni mji wa Kenya katika Bonde la Ufa la Afrika Mashariki. Ni makao makuu ya kaunti ya Trans-Nzoia.

Mji uko mita 1900 juu ya usawa wa bahari.

Hifadhi ya Taifa ya Saiwa Swamp iko karibu na mji, ambao unajulikana pia kwa makumbusho ya Kitale [1].

Mazao ya sokoni inayokuzwa katika sehemu hii ni majani ya chai, kahawa, pareto, alizeti, maharagwe na mahindi. Kitale ni soko la mazao ya kilimo na kituo cha kilimo cha mseto.

Mji huu ulianzishwa mwaka wa 1908 na Wazungu walowezi. Reli ya Uganda kutoka Eldoret ilifika Kitale mwaka wa 1926 na ilichangia kukuza mji huu. Kadiri ya sensa ya mwaka 2009, mji ulikuwa na wakazi 106,187[2].

Tazama pia

Marejeo

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2013-11-11. Iliwekwa mnamo 2010-08-29.
  2. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.

Viungo vya nje

Coordinates: 1°01′N 35°00′E / 1.017°N 35.000°E / 1.017; 35.000