Nenda kwa yaliyomo

Jumamosi kuu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu maarufu ya Pietà ya Michelangelo iliyochongwa katika marumaru kumuonyesha Bikira Maria akipakata maiti ya mwanae Yesu mara baada ya kifo chake msalabani.
Picha takatifu ya Jumamosi Kuu na Takatifu, ikimuonyesha Yesu Kushukia kuzimu.

Jumamosi kuu ni siku ya Juma kuu inayoadhimisha hasa pumziko la mwili wa Yesu Kristo kaburini na roho yake kushukia kuzimu kabla ya kufufuka kwa utukufu usiku wa kuamkia Jumapili ya Pasaka.

Tarehe yake inabadilikabadilika kila mwaka na hata mwaka uleule ni tofauti katika madhehebu ya Ukristo, hasa yanayofuata mapokeo ya mashariki na yale yanayofuata mapokeo ya magharibi.

Siku hiyo Misa na sakramenti mbalimbali haziadhimishwi kwa kuwa wafuasi wa Yesu wanatulia kimya wakitafakari matukio ya Ijumaa kuu na kujiandaa washangilie ufufuko wake kuanzia kesha la Pasaka hadi Jumapili ya Pentekoste siku 50 baadaye.

Majina katika lugha mbalimbali

[hariri | hariri chanzo]

Jumamosi kuu inaitwa kwa namna tofauti katika lugha mbalimbali. Baadhi ya mifano ni kama ifuatavyo:

LughaJinaTafsiri
KichekiBílá sobotaJumamosi nyeupe
KifaransaSamedi saintJumamosi takatifu
KihispaniaSábado SantoJumamosi takatifu
KiholanziStille ZaterdagJumamosi ya kimya
KihungariaNagyszombatJumamosi kuu
KiingerezaHoly SaturdayJumamosi takatifu
KiitaliaSabato SantoJumamosi takatifu
Kijapani聖土曜日 (Sei Doyoobi)Jumamosi takatifu
KijerumaniKarsamstagJumamosi ya ombolezo
KipolandiWielka SobotaJumamosi kuu
KislovakiaBiela sobotaJumamosi nyeupe
  • Parry, Ken (1999). The Blackwell Dictionary of Eastern Christianity. Malden, MA.: Blackwell Publishing. ISBN 0-631-23203-6. OCLC 156905118. {{cite book}}: Unknown parameter |coauthors= ignored (|author= suggested) (help)

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jumamosi kuu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.