Krisma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Chombo cha kioo chenye krisma ndani yake. Kwa juu imeandikwa SC, kifupi cha maneno ya Kilatini sanctum chrisma, yaani krisma takatifu.
Aina ya tabenakulo ya mafuta matakatifu vinapotunzwa kwa heshima krisma, mafuta ya wagonjwa na mafuta ya wakatekumeni.

Krisma (kutoka Kigiriki: χρῖσμα, Khrisma, yaani mpako) ni mafuta ya kunukia yanayotumiwa na Wakristo wa madhehebu mbalimbali (Wakatoliki, Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Wakatoliki wa Kale, Waanglikana, Wamormoni na baadhi ya Walutheri) katika ibada kadhaa, hasa sakramenti za ubatizo, kipaimara na daraja takatifu.

Krisma ndiyo asili ya majina Kristo, Wakristo yanayomtambulisha Yesu na wafuasi wake.

Ukristo wa Magharibi[hariri | hariri chanzo]

Askofu akiandaa krisma.

Kanisa la Kilatini[hariri | hariri chanzo]

Katika Kanisa la Kilatini mafuta ya zeituni yanachanganywa na manukato na kuwekwa wakfu na askofu akishirikiana na mapadri wa jimbo lake, kwa kawaida asubuhi ya Alhamisi kuu, baada ya kubariki mafuta ya wakatekumeni na yale ya wagonjwa.

Krisma ni ya lazima kwa sakramenti ya Kikatoliki ya Kipaimara, na inatumiwa pia katika sakramenti za Ubatizo na Daraja Takatifu.

Katika ubatizo, ikiwa mtu aliyebatizwa hatathibitishwa kwa Kipaimara mara moja, mhudumu humtia mafuta ya krisma utosini.

Wale waliowekwa wakfu kwa upadri, baada ya kupokea daraja hupakwa krisma kwenye mikono, na waliopewa uaskofu hutiwa mafuta kichwani na Askofu mwadhimishaji.

Pia hutumiwa katika utakaso wa vitu kama vile makanisa na madhabahu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Krisma kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.