Isaka wa Ninawi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Isaac of Nineveh)

Isaka wa Ninawi (kwa Kiaramu ܡܪܝ ܐܝܣܚܩ ܕܢܝܢܘ; kwa Kiarabu: إسحاق النينوي Ishak an-Naynuwī; kwa Kigiriki Ἰσαὰκ Σύρος, Isaac Syuros; kwa Kiingereza Isaac of Nineveh[1][2][3]; 613 hivi – 700 hivi) alikuwa mwanateolojia na askofu wa Kanisa la Asiria.

Ni maarufu hasa kwa maandishi yake juu ya maisha ya Kiroho. Yapo hadi leo katika lugha asili ya Kisiria na katika tafsiri za kale za Kigiriki na Kiarabu. Yametumiwa sana na Wakristo wa madhehebu mengine, hasa ya Mashariki.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, katika Kanisa lake na makanisa ya Waorthodoksi wa Mashariki na Waorthodoksi.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 28 Januari.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa Beth Qatraye, kati ya Mesopotamia na Arabia (Qatar ?)[4][5][6].

Akiwa bado kijana sana alijiunga na monasteri akafanya bidii sana. Akitumia pia maktaba iliyokuwepo, alijipatia sifa upande wa teolojia akaanza kufundisha dini katika eneo lake asili.

Patriarki Georges alipotembelea eneo hilo katikati ya karne ya 7 ili kushiriki sinodi, alimfanya Isaka kuwa askofu wa Ninawi, Assyria, mbali sana, katika Mesopotamia ya Kaskazini.[7].

Majukumu hayo mapya hayakufaa tabia yake, hivyo baada ya miezi 5 alijiuzulu akarudi kusini katika upweke wa Mlima Matout. Huko aliishi miaka mingi akila mikate 3 tu kwa juma pamoja na mboga kidogo.

Hatimaye uzee na upofu vilimlazimisha kurudi monasterini. Huko Shabar alifariki na kuzikwa.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Great Synaxaristes: Kigezo:Gr icon Ὁ Ὅσιος Ἰσαὰκ ὁ Σύρος Ἐπίσκοπος Νινευΐ. 28 Ιανουαρίου. ΜΕΓΑΣ ΣΥΝΑΞΑΡΙΣΤΗΣ.
  2. St Isaac the Syrian the Bishop of Nineveh. OCA - Lives of the Saints.
  3. Fromherz, Allen (2012). Qatar: A Modern History. I. B. Tauris. p. 43. ISBN 978-1-58901-910-2. 
  4. Markose, Biji (2004). Prayers and Fasts According to Bar Ebroyo (AD 1225/6-1286): A Study on the Prayers and Fasts of the Oriental Churches. LIT Verlag. p. 32. ISBN 9783825867959. 
  5. Kurian, George (2010). The Encyclopedia of Christian Literature, Volume 2. Scarecrow Press. p. 385. ISBN 081086987X. 
  6. Johnston, William M. (2000). Encyclopedia of Monasticism: A-L. Taylor & Francis. p. 665. ISBN 1579580904. 
  7. Kozah, Mario; Abu-Husayn, Abdulrahim; Al-Murikhi, Saif Shaheen; Al-Thani, Haya (2014). The Syriac Writers of Qatar in the Seventh Century (print ed.). Gorgias Press LLC. p. 263. ISBN 978-1463203559. 

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.