Maktaba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Maktaba ya Abasia ya Melk nchini Austria.
Halifax Central Library, mfano wa maktaba ya kisasa.
Ukumbi wa kujisomea katika maktaba ya New York City.

Maktaba ni sehemu au jengo lililo maalum kwa ajili ya kujisomea na kujifunza juu ya vitu mbalimbali. Kuna aina kadhaa za maktaba ila zote hazina tofauti kwani zina lengo moja: kutoa elimu.

Asilimia kubwa ya maktaba huwa na vitabu vya aina mbalimbali, kwa mfano: vya kiada na ziada.

Pia unaweza kuwa na maktaba yako binafsi na licha ya kuwa na maktaba yako unaweza kwenda shuleni ukaingia maktaba kwani kuna maktaba ya shule.

Pia kuna maktaba ya kijiji, ya wilaya, ya mkoa na hata ya taifa, zote hizi kwa ajili ya elimu.