Nyati wa Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyati wa Afrika
Nyati katika Hifadhi ya Mabula, Afrika Kusini
Nyati katika Hifadhi ya Mabula, Afrika Kusini
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Artiodactyla (Wanyama wenye vidole viwili au vinne mguuni)
Nusuoda: Ruminantia (Wanyama wanaocheua)
Familia: Bovidae (Wanyama walio na mnasaba na ng'ombe)
J. E. Gray, 1821
Nusufamilia: Bovinae (Wanyama wanaofanana na ng'ombe)
Jenasi: Syncerus (Nyati)
(Hodgson, 1847)
Spishi: S. caffer
(Sparrman, 1779)
Ngazi za chini

Nususpishi 5:

Msambao wa nyati wa Afrika
Msambao wa nyati wa Afrika

Nyati au mbogo (jina la kisayansi: Syncerus caffer) ni mnyama wa Afrika. Hana uhusiano wa karibu na nyati-maji wa Asia aliye mkubwa zaidi kidogo, lakini asili yake haieleweki. Kutokana na tabia yake isiyotabirika na inayomsababisha kuwa hatari sana kwa binadamu, nyati wa Afrika hafugwi, kinyume na mwenzake wa Asia.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Nyati ni mnyama mkubwa. Ana mita 1.7 kwenda juu, urefu wa mita 3.4.

Nyati wa savana ana uzito wa kilo 500–900, ambapo nyati wa kiume kwa kawaida huwa mkubwa kuliko nyati wa kike, akiwa na uzito wa juu mbalimbali. Nyati wa msitu huwa nusu ya kiwango hicho.[1]

Nyati wa savana huwa wa rangi nyeusi au kahawia nyeusi na pembe zao zimejikunja katika mpevu; nyati wa msitu nao huwa wa rangi ya kahawia nyekundu na pembe zao zimejikunja nyuma na juu.

Ndama wa aina zote mbili wana ngozi nyekundu.

Nususpishi[hariri | hariri chanzo]

Mazingira[hariri | hariri chanzo]

Kundi la nyati katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Tanzania.

Nyati wa Afrika ni mmoja wa wanyama maarufu walao nyasi katika Afrika. Wanaishi katika maeneo ya vinamasi, mbuga, na misitu ya milima mikuu ya Afrika. Nyati hupendelea makazi ya vichaka au matete manene, lakini wanapatikana pia katika mapori wazi.

Makundi makubwa ya nyati hupatikana katika maeneo ya miti na mapori. Nyati hawakai katika maeneo yaliyokanyagwa au kupunguzwa kwa muda mrefu.

Nyati huhitaji maji kila siku, kwa hiyo wanategemea vyanzo vya kudumu vya maji.

Kama punda milia, nyati hula manyasi marefu. Nyati hupunguza urefu wa nyasi ili zapendelewa na wanyama wengine walao nyasi. Wakati wa kula, nyati hutumia ulimi na meno yake mapana kula nyasi haraka kuliko wanyama wengine wa Afrika walao nyasi.

Maadui[hariri | hariri chanzo]

Zaidi na binadamu, nyati huwa na maadui wachache na wana uwezo wa kujikinga na simba, na hata kumwua.[2] Simba huwaua na kula nyati mara kwa mara, lakini kwa kawaida huchukua simba wengi kumwangusha nyati mzima mmoja. Mamba wa Nile kwa kawaida hushambulia nyati wazee na ndama tu.[3] Chui na fisi ni tishio tu kwa ndama mchanga, ingawa fisi wamerekodiwa kumwua nyati mzima wakati mwingine.[4]

Tabia za kijamii[hariri | hariri chanzo]

Ukubwa wa makundi ya nyati hubadilika sana. Makundi ya kawaida huwa na nyati wa kike wanaohusiana, pamoja na uzao wao, katika ukoo ambao hupangwa kwa hadhi. Makundi ya kawaida huzungukwa na makundi madogo ya madume ya cheo cha juu, madume ya chini, majike ya cheo cha juu na walio wazee. Madume vijana hukaa mbali na fahali atawalaye, ambaye hujulikana kutokana na ukubwa wa pembe zake.

Mafahali wanaojiandaa kushindana.

Mafahali wazima hushiriki katika michezo ya kupigana au vita halisi. Fahali mmoja atakaribia mwenzake, akikoroma, kichwa chake chini, na kusubiri mwenzake kufanya hivyo. Mafahali hao wanapopigana hugeuza pembe zao kushoto na kulia. Ikiwa vita hivyo vina madhumuni ya kucheza, mafahali husuguana uso na miili katika mchezo huu. Vita halisi ni vikali, lakini ni vya nadra na vifupi. Ndama pia wanaweza kushindana, lakini ni nadra kwa nyati wa kike kushindana hivyo.

Wanapokimbizwa na wanyama wa kuwinda, nyati hukaa pamoja kwenye kikundi ili kufanya kuwa ngumu kwa wanyama wa kuwinda kunyang'anya mmoja wao. Ndama hukusanyika katikati. Nyati atajaribu kumnusuru mwenzake aliyeshikwa. Wito wa ndama hupata uangalifu wa mama na pia kundi lote. Nyati hupigana wakiwa wengi wanapopigana na wanyama wa kuwinda. Wamerekodiwa kuwakimbiza simba juu ya mti na kuwasumbua kwa masaa mawili, baada ya simba kuua nyati mwenzao. Inawezekana kwa watoto wa simba kukanyagwa na kuuawa na nyati. Katika tukio lililochukuliwa na picha, ndama alinusurika aliposhambuliwa na simba wachache na mamba baada ya kusaidiwa na kundi.

Uzazi[hariri | hariri chanzo]

Nyati wa Afrika na ndama wake.

Nyati hujamiiana na kujifungua wakati wa mvua peke yake. Kilele cha kuzaa huwa mwanzoni wa msimu na kilele cha kujamiiana huwa baadaye. Fahali atakaa karibu na nyati aliye na joto na pia kuweka mafahali wenzake mbali. Hii ni vigumu kabisa kwani nyati huwavutia madume wengi katika eneo hilo. Wakati jike yuko tayari kabisa, fahali tu aliye na nguvu kabisa ndiye hubakia kule.

Majike huzaa mara ya kwanza baada ya miaka mitano, baada ya kipindi cha mimba miezi 11.5. Ndama waliozaliwa hufichwa katika vichaka kwa wiki chache za kwanza wakitunzwa na mama zao kabla ya kujiunga na kundi kuu. Ndama huwa katikati ya kundi kwa ajili ya usalama.[5]

Uhusiano wa mama na ndama hudumu muda mrefu zaidi kuliko wanyama wengi walao majani. Hata hivyo wakati ndama mpya anapozaliwa, ule uhusiano unaisha na mama yake huwaweka mbali watoto wengine kwa kutumia pembe.

Nyati wa kiume huacha mama zao wanapokuwa na umri wa miaka miwili na kujiunga na vikundi vya mafahali walio wachanga.

Uhusiano na binadamu[hariri | hariri chanzo]

Nyati katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, Tanzania.

Hali[hariri | hariri chanzo]

Hali ya sasa ya nyati wa Afrika hutegemea kuwepo wawindaji wa wanyama wa thamani na watalii wawindaji, wakiingilia harakati za kuhifadhi kupitia doria ya urekebishaji wa uharibifu wa mazao kijijini, na programu za marekebisho ya maeneo ya CAMPFIRE.

Nyati wafugwao nchini Kenya katika jua kuchwa.

Idadi jumla ya nyati imeenea maeneo yote isiyo jangwa katika Afrika, kutoka kusini mwa Chad mpaka Afrika ya Kusini. Idadi ya nyati inakadiriwa karibu milioni moja, lakini hesabu sahihi haiwezekani kwani hakuna usaidizi wa fedha za kufanyia utafiti katika maeneo kama vile Sudan, Chad, Kongo na Benin. Wengi wa wawindaji wataalamu, wanaosafiri, na wataalamu wa wanyamapori huamini kuwa idadi hii inawakilisha nyati kusi, bila kuhesabu nyati wa naili, nyati-milima, au nyati-msitu.

Mashambulizi[hariri | hariri chanzo]

Kama mmoja wa "Wakubwa tano" au "Kifo cheusi" katika Afrika, nyati wa Afrika anajulikana kama mnyama hatari sana, wakiua watu zaidi ya 200 kila mwaka. Nyati wakati mwingine huripotiwa kuua watu zaidi katika Afrika kuliko mnyama mwingine yeyote, ingawa wakati mwingine hudaiwa kusababishwa na kiboko au mamba.[6] Nyati huwa na sifa mbaya miongoni mwa wawindaji kama mnyama hatari sana, kwa sababu ya wanyama waliojeruhiwa wakiripotiwa kuvizia na kushambulia wawindaji.[7]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Angalia pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Syncerus caffer.
  2. Cape Buffalo. Canadian Museum of Nature.
  3. Syncerus caffer - Nyati wa Afrika
  4. Kruuk, Hans (1972). The Spotted Hyena: A study of predation and social behaviour. New York: Parkwest. p. 335. ISBN 0563208449. 
  5. African Buffalo. British Broadcasting Corporation. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-05-31. Iliwekwa mnamo 2010-01-06.
  6. Africa on the Matrix: The Cape Buffalo. Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-04-20. Iliwekwa mnamo 2010-01-06.
  7. African Animals Hunting facts and tips - Buffalo Hunting. Jalada kutoka ya awali juu ya 2013-07-08. Iliwekwa mnamo 2010-01-06.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Estes, R. (1991). Mwelekezo wa tabia za Mamalia kutoka Afrika, pamoja na mamali wenye kukla nyama na wenye kufanana na binadamu. Los Angeles,Shirika la chuo kikuu cha kalifonia la uchapishaji
  • Ikolojia na tabia ya Nyati wa Afrika - Kutokuwa sawa kijamii na maamuzi (Chapman & Hall Wildlife ikolojia & tabia)
  • Huffman, B. 2006. Ukurasa maalum wa Ungulate. UltimateUngulate.com. ilirekebishwa 11 Januari 2007.
  • Umoja wa kimataifa kwa ajili ya Uhifadhi wa hali na Maliasili (IUCN). 2006. Syncerus caffer, Archived 23 Septemba 2008 at the Wayback Machine.
  • Nowak, RM na Paradiso, JL 1983. Walker Mamalia wa Dunia. Baltimore, Maryland, USA: Shirika la chuo kikuu cha Johns Hopkins la uchapishaji. ISBN 0-8018-2525-3

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.