Nyasi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyasi
Nyasi
Nyasi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Monocots (Mimea ambayo mche wao una jani moja)
(bila tabaka): Commelinids (Mimea kama jaja)
Oda: Poales (Mimea kama nyasi)
Familia: Poaceae (Nyasi)
Ngazi za chini

Nusufamilia 12

Nyasi ni kundi la mimea inayofunika udongo; nyasi zilizo nyingi si kubwa sana lakini aina kama mianzi hufikia urefu wa miti. Kibiolojia hujumlishwa katika familia ya Poaceae au Gramineae.

Nyasi nyingi huwa na mizizi mirefu inayoshika ganda la juu la ardhi hivyo kuzuia au kupunguza mmomonyoko wa udongo. Kiekolojia aina za nyasi zimezoea mazingira tofauti kabisa kati ya kanda za joto hadi kanda za baridi sana. Wakati wa baridi au ukame majani juu ya ardhi hukauka hata kupotea kabisa lakini mizizi ina uwezo wa kulala muda mrefu na kusubiri mvua au halijoto ya juu zaidi.

Lishe ya wanyama[hariri | hariri chanzo]

Watu wametumia nyasi kwa shughuli mbalimbali. Nyasi ni muhimu kama lishe ya wanyama kama ng'ombe au kondoo. Wanyamapori wengi wanakula nyasi vilevile. Wakulima wanaweza kuteua aina za nyasi zinazofaa kama lishe ya mifugo na kuzipanda. Kumekuwa sababu mbalimbali toka kwa wanasayansi kuelezea kwa nini binadamu hali nyasi.[1]

Ng'ombe wakila nyasi karibu na Hradec nad Moravicí huko Silesia ya Ucheki.

Nafaka, viungo na dawa[hariri | hariri chanzo]

Aina kadhaa za nyasi hutoa mbegu zinazoliwa na watu kama nafaka; nyasi hizo za nafaka kama vile mahindi, mpunga au ngano ni kati ya vyakula vya msingi vya binadamu duniani kote. Asilimia 70 ya mimea yote inayopandwa ni nyasi.[2]. Aina nyingine za nyasi hutumika pia kama dawa za aina mbalimbali kwa binadamu na viungo vya chakula au vinywaji kama chai.

Mimea kwa burudani[hariri | hariri chanzo]

Katika mazingira ya mjini nyasi za pekee hutumiwa kufunika ardhi hasa katika maeneo ya bustani yanayokanyagwa na watu wengi wanapenda kukalia kwenye nyasi na kupumzika; aina hizi zinatumiwa pia kwenye viwanja vya michezo. Katika bustani nyasi hukatwa kwa mitambo maalum kuwa fupi ili kupendezesha bustani, tofauti na nyasi za mashambani au sehemu za kulishia wanyama.[3] Nyasi hutumika pia kufunika ardhi nje ya nyumba ili kuipendezesha.

Nyasi mbele ya nyumba.

Ujenzi[hariri | hariri chanzo]

Nyasi hutumika pia kwa ujenzi wa nyumba, mara nyingi maeneo ya vijijini, hasa katika nchi zinazoendelea.

Nyumba imefunikwa na nyasi nchini Iceland.

Majina ya aina za nyasi katika Afrika ya Mashariki[hariri | hariri chanzo]

Nyasi-bahari zinafanana na nyasi za kweli za oda Poales lakini zinaainishwa katika oda Alismatales. Pwani ya Afrika ya Mashariki ina spishi 12 katika jenasi 8.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Kwa nini binadamu hakuli nyasi?
  2. George Constable, ed. (1985). Grasslands and Tundra. Planet Earth. Time Life Books. p. 19. ISBN 0-8094-4520-4. 
  3. "mitambo ya kukata majani

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]