Mwanzi (nyasi)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwanzi
(Bambuseae)
Msitu wa mianzi huko Japani
Msitu wa mianzi huko Japani
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Monocots (Mimea ambayo mche wao una jani moja)
(bila tabaka): Commelinids (Mimea kama jaja)
Oda: Poales (Mimea kama manyasi)
Familia: Poaceae (Mimea iliyo mnasaba na manyasi)
Nusufamilia: Bambusoideae
Ngazi za chini

Makabila 3:

Mwanzi ni jina la spishi nyingi za nyasi ndefu zinazoweza kuonekana kama miti. Mianzi yote huwa na shina ya aina ya ubao.

Mianzi hupatikana kiasili katika Afrika, Amerika na Asia lakini inastawi pia ikipandwa Ulaya.

Urefu wa spishi kubwa hufikia kina cha mita 40. Inaweza kukua zaidi ya mita 1 kila siku lakini kwa kawaida ni sentimita 3-5 kwa siku.

Shina la mianzi huwa na umbo la bomba na unene wake ni hadi sentimita 30. Shina hugawiwa na vifundo. Kila kifundo kina chipukizi na machipukizi yanaweza kuendelea kuota matawi.

Matumizi[hariri | hariri chanzo]

Mianzi ina matumizi mengi kwa binadamu. Inafaa kwa ujenzi wa nyumba, madaraja au maboti. Mashina hutumika pia kwa mabomba ya maji katika nyumba na kilimo.

Wakati ni changa na laini yaani kabla ya kuwa ubao mwanzi unafaa kama chakula baada ya kupikwa. Mtovu unakusanywa pia kama kinywaji hasa ulanzi.

Katika utamaduni wa China ya Kale vipande vya mianzi vilitumiwa kama bao za kuandika matini.

Nyuzi zake hutumika pia kutengeneza magodoro.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mwanzi (nyasi) kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.