Okapi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Okapi
Okapi
Okapi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Mamalia - wanyama wanaonyonyesha watoto wao)
Oda: Artiodactyla (Mamalia wanaokanyaga kwa kwato mbili-mbili)
Familia: Giraffidae (Mamalia walio na mnasaba na twiga)
Jenasi: Okapia (Okapi)
Lankester, 1901
Spishi: O. johnstoni
Sclater, 1901
Msambao wa okapi
Msambao wa okapi

Okapi (jina la kisayansi: Okapia johnstoni) ni mamalia wa familia ya twiga. Umbo lake hufanana na farasi ina michoro miguuni kama punda milia lakini haina uhusiano naye, ni aina ya twiga.

Okapi ni mnyama aliyejulikana na wenyeji wa maeneo yake tu hadi mwaka 1901. Hapo zamani ilikuwa inaaminika kuwa mnyama huyu hupatikana tu katika misitu ya Ituri lakini mwaka 2006 zilipatikana dalili zilizoonyesha kwamba mnyama huyu yuko pia kwenye misitu ya hifadhi ya taifa ya Kongo ya Virunga. Kwenye misitu ya Ituri kuna hifadhi ya Okapi yenye eneo la km² 14,000.

Shingo yake ni fupi kuliko twiga lakini ina ulimi mrefu sana wa kujipatia majani unaomwezesha kusafisha masikio yake yeye mwenyewe. Dume ina pembe mbili fupi kichwani.

Kimo cha okapi ni hadi mita 2.5 kichwani na hadi mita 2 mabegani. Anafikia uzito kati ya kg 200 hadi 250. Anakula majani ya miti pamoja na nyasi, matunda na nyoga.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.