İzmir

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pwani ya Izmir.

İzmir, kwa jina la kihistoria Smyrna, ni mji wa tatu kwa ukubwa katika Uturuki, na ndio mji wenye bandari kubwa baada ya Istanbul. Upo katika eneo la maji yatokayo Ghuba ya İzmir, katika Bahari ya Aegean.

Huu ni mji mkuu wa Mkoa wa İzmir, ambao una eneo la kilomita za mraba zipatazo 7350.

Mji wa İzmir una wilaya zipatazo kumi. Wilaya hizo ni pamoja na Balçova, Bornova, Buca, Çiğli, Gaziemir, Güzelbahçe, Karşıyaka, Konak, Menemen, na Narlıdere, ambazo kila moja ni tofauti sana na nyingine.

Kanisa la Smirna ni kati ya yale saba ambayo yaliandikiwa barua katika Ufunuo wa Yohane, kitabu cha mwisho cha Agano Jipya na cha Biblia ya Kikristo. Ndilo linalosifiwa zaidi, hasa kutokana na kiongozi wake, askofu Polikarpo wa Smirna.

Idadi ya wakazi kwa miaka[hariri | hariri chanzo]

Idadi ya watu wa İzmir
Mwaka Idadi
2007 2,606,294
2000 2,232,265
1990 1,758,780
1985 1,489,817
1970 554,000
1965 442,000
1960 371,000
1955 286,000
1950 231,000
1945 200,000
1940 184,000
1935 171,000
1927 154,000

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu İzmir kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.