Şanlıurfa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtaa wa mji.

Şanlıurfa (mara nyingi na katika lugha ya kila siku hujulikana kwa jina fupi kama Urfa; au kwa Kiaramu; Riha au Urhāy, kwa Kiarmenia Urhai, kwa Kiarabu الرها al-Raha; zamani ulikuwa ukitajwa kama Edessa) ni mji wenye wakazi takriban 462,923 (makadirio ya mwaka wa 2006[1]).

Mji upo kilomita 80 upande wa mashariki mwa mto Frati, kusini-mashariki mwa nchi ya Uturuki, na ndio makao makuu ya Mkoa wa Şanlıurfa.

Hali ya hewa ni ya joto mno, kiangazi kikavu na baridi kiasi.

Idadi kubwa ya wakazi wa mji ni Wakurdi wakati maeneo mengine ya kanda kuna mchanganyiko wa Waarabu na Waturuki na idadi ndogo kabisa ya Wazaza, Wayezidi, Waarmenia na Wayahudi.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Turkey Population statistics Archived 6 Agosti 2009 at the Wayback Machine. Retrieved on 2009-06-30.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Şanlıurfa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.