Mkoa wa İzmir

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkoa wa İzmir
Maeneo ya Mkoa wa İzmir nchini Uturuki
Maelezo
Kanda: Kanda ya Aegean
Eneo: 11,973 (km²)
Idadi ya Wakazi 3,769,000 TUIK 2007 (est)
Kodi ya Leseni: 35
Kodi ya eneo: 0232
Tovuti ya Gavana http://www.i̇zmir.gov.tr
Utabiri wa hali ya hewa turkeyforecast.com/weather/i̇zmir

İzmir ni jina la kutaja moja kati ya Mikoa ya Uturuki uliopo mjini magharibi mwa Anatolia kwenye pwani ya Bahari ya Aegean. Mji mkuu wa mkoani hapa ni Izmir. Mji huu ulianzishwa na Wagiriki Smyrna (Kigiriki: Σμύρνη) kunako karne ya 11 KK. Kwa upande magharibi umezungukwa na Bahari ya Aegean, na imefungamana kabisa na Ghuba ya İzmir. Mkoa umechukua eneo la kilomita za mraba zipatazo 11,973. Takriban watu 3,769,000 wanaishi mjini hapa (makisio ya 2007). Idadi ya wakazi wa hapa ilikuwa 3,370,866 kunako mwaka wa 2000. Mikoa ya jirani na mkoa ni pamoja na Balıkesir katika upande wa kaskazini, Manisa kwa upande wa mashariki, na Aydın kwa upande wa kusini.

Wilaya za mkoani hapa[hariri | hariri chanzo]

Mkoa wa İzmir umeganyika katika wilaya zipatazo 30 (mji mkuu umekoozeshwa):

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa İzmir kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.