Bahari ya Aegean

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Coordinates: 39°N 25°E / 39°N 25°E / 39; 25

Bahari ya Aegean.

Bahari ya Aegean (pia: Aegeis; tamka a-e-ge-is) ni moja kati ya sehemu za Bahari ya Mediteranea. Ipo kati ya Ugiriki na Anatolia (Uturuki).

Kupitia mlangobahari wa Dardaneli imeungana na Bahari ya Marmara, Bosporus na Bahari Nyeusi.

Jina[hariri | hariri chanzo]

Jina la bahari hii kwa Kigiriki wanaliita Αἰγαῖον Πέλαγος (Aigaion Pelagos), Kigiriki cha kisasa: Αιγαίο Πέλαγος (Aigaio Pelagos). Kwa jina la Kituruki ni Ege Denizi.

Watu wengi wa kale walikuwa wakifikiria tofauti kuhusu jina hili, kwa nini wameiita Aegean.

Labda lilitolewa kufuata mji wa Aegae, au Aegea, ambaye ni malkia wa Amazoni aliyekufa katika bahari hiyo.

Labda lilitolewa kufuata Aegeus, baba wa Theseus shujaa wa Ugiriki ya Kale. Hadithi za kale zinasema kwamba Aegeus alijiua pale alipofikiria kuwa mtoto wake wa kiume amekufa katika bahari hiyo.

Kuna baadhi ya watu wanasema kwamba jina hili linatoka chimbuko la lugha ndogondogo (neno) αἶγες (aiges) au "mawimbi" .

Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bahari ya Aegean kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.