Mange Kimambi
Mange Jumanne Ramadhan Kimambi (alizaliwa mkoa wa Arusha, 1980) ni mmoja wa wanawake wanaharakati wenye ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii katika nchi ya Tanzania.
Mange Jumanne Ramadhan Kimambi kabila lake ni Mpare na ameolewa nchini Marekani na Mzungu raia wa Marekani na wamebahatika kupata watoto wawili wa kiume. Hadi sasa inasemekana amekuwa akiishi jijini Los Angeles nchini Marekani tangu mwaka 2008.[1] [2].
Elimu
Mange Kimambi alipata elimu ya msingi katika Shule ya msingi Arusha; baadaye alichaguliwa kujiunga na shule ya sekondari Arusha lakini alipelekwa na baba yake kusoma elimu hiyo katika jiji la Harare nchini Zimbabwe.
Baada ya kuhitimu elimu ya sekondari Mange Kimambi alipata nafasi ya kwenda nchini Marekani kwa ajili ya masomo ya juu, lakini wakati akiwa masomoni alipata ujauzito na kujifungua mtoto wa kike aitwaye Bhoke.
Baadaye aliamua kurejea nchini Tanzania ili kujipanga tena kwa ajili ya kuendelea na shule. Dada huyu alifanikiwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mnamo mwaka 2004 ambapo alisoma na kutunukiwa shahada ya Business Administration. Baada ya kupata shahada alikwenda Dubai katika Falme za Kiarabu ambapo alisoma na kupata shahada ya uzamili(MBA).
Siasa
Tangu alipoanza kujihusisha na siasa alifikia hatua ya kusema hajui maisha yake yangekuaje bila CCM.[onesha uthibitisho] Lakini amejipatia umaarufu zaidi kuanzia mwaka 2016 mara baada ya serikali ya awamu ya tano iliyokuwa ikiongozwa na Rais John Pombe Magufuli kuingia madarakani. Umaarufu wa Mange Kimambi umetokana na uthubutu wa kupinga waziwazi mambo mengi yanayofanywa na serikali iliyo chini ya chama tawala CCM. Hatua hiyo ikawa tokeo la kufuatiliwa na watu wengi katika Instagram.
Alisifika pia kwa kuratibu maandamano ya Watanzania wanaoishi Marekani.[3] Pia kuwa sehemu kubwa ya mratibu wa maandamano ya tarehe 29 Oktoba 2025.[4]
Tanbihi
- ↑ "Who Is Mange Kimambi? Jua ukweli wenye facts sio grapevine kumhusu huyu mtu, biography and facts! - JamiiForums". JamiiForums (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2018-09-10.
- ↑ YOUR-NAME, "Makala : Mange Kimambi ni Nani? Kumbe kasoma Arusha? Na Jeff Msangi.", Wazalendo 25 Blog (kwa American English), iliwekwa mnamo 2018-09-10
- ↑ "MANGE KIMAMBI AUMBUKA BAADA YA MAANDAMANO KUKOSA WADAU MAREKANI". Iliwekwa mnamo 2025-11-08.
- ↑ Tanzania,Pad.Kitima:vifo vingi katika maandamano.Jitihada ya Kanisa katika mazungumzo - | Vatican News
Viungo vya nje
- https://wazalendo25.blogspot.com/2017/03/makala-mange-kimambi-ni-nani-kumbe.html
- https://www.jamiiforums.com/threads/who-is-mange-kimambi-jua-ukweli-wenye-facts-sio-grapevine-kumhusu-huyu-mtu-biography-and-facts.693066/
| Makala hii kuhusu kuhusu mwanasiasa wa Tanzania bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mange Kimambi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |