Zizi la kuku

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Zizi la kuku.
Mayai ndani ya zizi la kuku.

Zizi la kuku au nyumba ya kuku ni nyumba maalumu ambayo kuku au aina nyingine ya ndege huhifadhiwa.

Zizi la kuku kwa kawaida lina eneo la ndani ambalo kuku unaweza kulala pamoja na eneo la nje ambalo kuku kutumia muda mwingi kutafuta chakula na kupumzika. Zizi la kuku kawaida hutakiwa kusafisha kila baada ya wiki mbili, na majani na nyasi kubadilishwa kila siku. Usiku kuku hufungiwa ndani ya zizi ili kuwalinda toka kwa maadui kama vile mbwa mwitu na paka. Sakafu ya zizi la kuku kawaida hufunikwa na nyasi na vumbi la mbao.

Dhumuni[hariri | hariri chanzo]

Lengo la kuku la kuku ni kulinda kuku kutokana na hali mbaya ya hewa - joto, baridi, upepo na mvua na kuwalinda kutoka kwa maadui zake - hasa mbweha na paka.

Utata[hariri | hariri chanzo]

Kumekuwa na utata wa muda mrefu kuhusu mahitaji ya msingi ya zizi la kuku. Falsafa moja, inayojulikana kama "shule ya hewa safi" inasema kwamba kuku wanaweza kuathiriwa na kitendo cha kufungiwa ndani, hewa chafu na giza, hivyo zizi la kuku linatakiwa kuwa na sehemu nzuri ya kupitisha hewa na mwanga. Zizi linapaswa kuwa kama vile mazingira ya nje yalivyo hata wakati wa majira ya baridi[1]. Hata hivyo, wengine wanasema kuwa kuku wakikaa nje ni rahisi kupata magonjwa kutokana na hali ya hewa nje.

Hii imesababisha miundo miwili ya zizi la kuku: zizi lenye hewa safi lililozungukwa tu na uzio (hata wakati wa baridi), au zizi lenye milango na madirisha. Hata hivyo, wataalamu wanakubaliana kuwa hewa safi ni muhimu kwa afya ya kuku. Zizi lisilo na hewa safi linaweza kusababisha kiharusi na pia kuwepo kwa hewa ya sumu zizini.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]