Upepo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro wa Pieter Kluyver (18161900) ukionyesha upepo mkali.
Alama za upepo usoni mwa maji.

Upepo ni mwendo wa hewa. Husababishwa na joto la jua. Hewa ikipashwa joto na jua hupanuka huwa nyepesi na kupanda juu. Hivyo inaacha nafasi ambako hewa baridi zaidi inaingia kuchukua nafasi yake.

Kwa lugha ya metorolojia kuna mwendo kutoka eneo la shindikizo la juu la hewa kwa eneo lenye shindikizo duni la hewa.

Kuna aina nyingi za upepo. Upepo mkali huitwa dhoruba. Ikizunguka ndani yake ni tufani, na tufani ikianza baharini ni kimbunga.

Nguvu ya upepo ilitumiwa na binadamu tangu karne nyingi kwa njia ya teknolojia mbalimbali kama vile

Tangu karne ya 20 nguvu ya upepo imetumiwa pia kutengeneza umeme. Katika karne ya 21 umeme wa upepo umeanza kuwa chanzo muhimu wa nishati.

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Upepo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.