Tufani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya rada ya tufani upande wa kaskazini ya ikweta
Picha ya tufani jinsi inavyoonekana kutoka kituo cha anga

Tufani (kutoka neno la Kiarabu) ni dhoruba yenye mwendo wa kuzunguka. Inasababishwa na eneo la shindikizo duni la hewa ambako upepo umeanza kuzunguka ndani yake.

Mzunguko huu hufuata mwendo wa saa katika maeneo ya kusini kwa ikweta na huenda kinyume cha mwendo wa saa katika maeneo ya kaskazini kwa ikweta.

Chamchela na Kimbunga[hariri | hariri chanzo]

Tufani ikitokea kwenye nchi kavu huitwa chamchela.

Kwenye bahari za tropiki mzunguko unaongezeka nguvu kutoka nishati ya joto ya maji baharini kuwa dhoruba kali. Tufani hizi zinazoanza baharini huitwa kimbunga. Kimataifa kuna majina mengine yaliyo tofauti kila bahari kama vile:

  • Katika eneo la Atlantiki (hasa Karibi) kimbunga huitwa hurikan (kwa Kiingereza Hurricane)
  • katika eno la Pasifiki Kaskazini kimbunga huitwa taifuni (en: typhoon)
  • katika eneo la Bahari Hindi na Pasifiki Kusini jina la saikloni (en: cyclone) limetumiwa

Tufani katika anga ya nje[hariri | hariri chanzo]

Tufani zimetazamwa pia katika falaki kwenye sayari za mfumo wa jua letu kama Mshtarii na Meriki. Hasa doa jekundu kubwa lililoonekana kwenye Mshtarii tangu mwaka 1830 na hata kabla ya hapo limetambuliwa kuwa tufani.

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tufani kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.