Kigonigoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kigonigoni ni kata ya Wilaya ya Mwanga iliyopo karibu na mpaka wa Kenya katika Mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania.

Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2022, kata ilikuwa na wakazi wapatao 3,325 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 2,610 [2] walioishi humo. Aidha Kigonigoni ndiyo makao makuu ya tarafa ya Jipendea.

Ndiyo kata yenye shule ya Advanced Level kwa upande wa tambarare ya mashariki.

Vijiji[hariri | hariri chanzo]

Kata ina vijiji vinne, ambavyo ni: Kigonigoni, Butu, Kwakihindi na Ruru.

Shughuli[hariri | hariri chanzo]

Shughuli kubwa za wakazi wa kata hii ni kilimo, ufugaji na uvuvi ndani ya Ziwa Jipe.

Kijiji ambacho wananchi wake wanajishughulisha na uvuvi kwa asilimia 90 ni kijiji cha Ruru.

Makabila[hariri | hariri chanzo]

Kabila kubwa linalopatikana katika kata hii ni Wapare. Yapo makabila mengine kama Wakamba na Wachaga ingawa makabila hayo ni kama yamemezwa na Wapare.

Dini[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wengi ni wafuasi wa dini ya Uislamu na ya Ukristo.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Watu wake hupendelea mlo wa ugali kwa samaki mara nyingi pamoja na makande, kutembeleana wakati wa sikukuu za kidini, Kushirikiana shughuli za msiba au ugonjwa.

Michezo kwao ni mpira wa miguu hasa kwa walio vijana zaidi.

Mipaka[hariri | hariri chanzo]

Upande wa mashariki kata hii inapakana na nchi ya Kenya, mwambao wa ziwa Jipe. Upande wa magharibi inapakana na safu ya milima ya Upare (Usangi). Upande wa kaskazini inapakana na kijiji cha Mkisha. Upande wa kusini inapakana na vijiji vya Kwakoa na Toloha.

Vivutio[hariri | hariri chanzo]

1. Ndiva yefuka katika Mto Mala. 2. Ziwa Jipe mpakani mwa Kenya na Tanzania.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz
  2. Sensa ya 2012, Kilimanjaro - Mwanga DC. Jalada kutoka ya awali juu ya 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2016-05-27.
Kata za Wilaya ya Mwanga - Mkoa wa Kilimanjaro - Tanzania

Chomvu | Jipe | Kifula | Kighare | Kigonigoni | Kileo | Kilomeni | Kirongwe | Kirya | Kivisini | Kwakoa | Lang'ata | Lembeni | Mgagao | Msangeni | Mwanga | Mwaniko | Ngujini | Shighatini | Toloha

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kigonigoni kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Isipokuwa usitaje majina ya viongozi waliopo sasa maana wanabadilika haraka mno.