Burka

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wanawake kwenye soko nchini Afghanistan wakivaa wamevaa burka.

Burka (pia burqa, kutoka Kiar. برقع‎) ni vazi la wanawake linalofunika mwili wote pamoja na kichwa na uso. Burqa huvaliwa na wanawake Waislamu katika maeneo kadhaa ambako ni utamaduni wa kawaida. Katika Afghanistan wanawake walilazimishwa kuivaa chini ya utawala wa Taliban kila walipotoka kwenye nyumba. Majina mengine ya burqa ni "chadori" katika Afghanistan na "paranja" katika nchi jirani za Asia ya Kati kama Tajikistan na Uzbekistan.

Wafuasi wa Uislamu wa mwelekeo wa Salafi mara nyingi wanadai eti ni lazima mwanamke kufunika uso wote akitoka nje ya nyumba anapoweza kuonekana kwa wanaume wasio wa familia yake.

Vazi linalofanana na burka huvaliwa pia na wanawake wa kundi dogo la Wayahudi wenye itikadi kali nchini Israeli.[1]

Vazi lingine la kufunika uso ni nikabu iliyotumiwa Uarabuni na kati ya wanawake wanaofuata itikadi ya Salafi kali. Lakini nikabu haifuniki macho, tofauti na burka. Wataalamu Waislamu wengi hawakubali sharti la kufunika uso wa wanawake [2][3] [4].

Nchi zinazokataza uvaaji wa burka;
Nyekundu nyeusi: Uvaaji wa hadharani unakatazwa kote
Njano: Uvaaji unakatazwa katika maeneo kadhaa
Pinki: Uzalishaji na biashara hukatazwa
Zambarau: Hukatazwa katika majengo ya serikali na mahali pa kazi.

Nchi kadhaa zimekataza kuvaa burka nje ya nyumba zikiwa na sheria zinazokataza mavazi zinazofunika uso, kwa mfano Austria, Ufaransa, Ubelgiji, Denmark, Bulgaria [5][6][7] Luxemburg,[8] Uswisi,[9] Gabon, Chad, Senegal[10][11], Sri Lanka[12], Tajikistan,[13] Uzbekistan[14], na China[15]. Katika nchi nyingi hairuhusiwi kutumia usafiri wa umma au kuingia katika shule, vyuo au majengo ya serikali ukiwa na vazi linalofunika uso.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. The ultra Orthodox Jewish sect where women cover themselves from head to toe (English). EFE (9 March 2017).
  2. Juan Eduardo Campo, ed. (2009). "Burqa". Encyclopedia of Islam. Infobase Publishing. ISBN 9781438126968 . https://books.google.com/books?id=OZbyz_Hr-eIC&pg=PA119. Retrieved 27 December 2018.
  3. Is Wearing the Niqāb Obligatory for Women?. Jalada kutoka ya awali juu ya 2014-07-09. Iliwekwa mnamo 2021-08-20.
  4. Hadia Mubarak (2009). "Burqa". In John L. Esposito. The Oxford Encyclopedia of the Islamic World. Oxford: Oxford University Press.
  5. "The Islamic veil across Europe", BBC News, 2018-05-31. 
  6. Where are 'burqa bans' in Europe? (en-GB) (1 August 2019).
  7. Tan, Rebecca. "From France to Denmark, bans on full-face Muslim veils are spreading across Europe", Washington Post, August 16, 2018. (en-US) 
  8. Alexandra Parachini. Le Luxembourg a désormais sa loi burqa | Le Quotidien (fr-FR).
  9. "Switzerland referendum: Voters support ban on face coverings in public", BBC News, 2021-03-07. (en-GB) 
  10. "The veil in west Africa - Banning the burqa", The Economist, 2016-02-11. 
  11. Après le Tchad et le Cameroun, le Sénégal renonce à la burqa et à ses suppôts (fr-FR) (2015-11-20).
  12. Colombo, Associated Press in (2021-03-13). Sri Lanka to ban burqa and close 1,000 Islamic schools (en).
  13. Tajikstan passes law 'to stop Muslim women wearing hijabs' (en) (2017-09-01).
  14. Reuters Staff. "Uzbek imam sacked after urging president to allow hijabs, beards", Reuters, 2018-09-10. (en) 
  15. "China bans burqa in capital of Muslim region of Xinjiang", 13 January 2015. 
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.