Mtume Mathayo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtume Mathayo
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Mathayo (kwa Kiebrania מַתִּתְיָהוּ, Mattityahu au מתי, Mattay, Zawadi ya Mungu; kwa Kigiriki Ματθαῖος, Matthaios) alikuwa Myahudi wa karne ya 1, mmojawapo kati ya Mitume wa Yesu anayeheshimiwa hasa kutokana na Injili yenye jina lake. Labda aliitwa pia Lawi.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Kabla hajaitwa na Yesu Kristo amfuate, Mathayo alikuwa mtozaushuru, na kwa sababu hiyo alitazamwa na Wayahudi kama msaliti wa taifa na mkosefu.

Hata hivyo Yesu alipomkuta forodhani alimuambia, "Nifuate" (Injili ya Marko 2:14). Ndipo Mathayo akaacha vyote akaanza kuwa mwanafunzi wake. Katika nafasi hiyo alimuandalia karamu kubwa waliyoishiriki watozaushuru wengi, hata kusababisha lawama kwa Yesu toka kwa Mafarisayo.

Inasemekana kwamba baada ya ufufuko wa Yesu, Mathayo alieneza habari njema Ethiopia, ingawa masalia yake yanaheshimiwa huko Salerno (Italia) tangu mwaka 954.

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Kuna ushahidi wa zamani kwamba aliwahi kuandika misemo ya Yesu kwa lugha ya Kiaramu. Kitabu hicho kilipotea mapema, na ni vigumu kusema kina uhusiano gani na Injili ya Mathayo iliyoandikwa moja kwa moja kwa Kigiriki fasaha.

Heshima baada ya kifo[hariri | hariri chanzo]

Wakristo wa madhehebu yote wanamheshimu kama mtakatifu, hasa tarehe 21 Septemba[1] na 16 Novemba.

Anaheshimiwa kama msimamizi wa watu wa benki, forodha, watunzahesabu n.k.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtume Mathayo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.