Yakobo Mkubwa
Yakobo, mwana wa Zebedayo na Salome, na kaka wa Mtume Yohane, alikuwa mmoja kati ya Mitume wa Yesu muhimu zaidi.
Anaitwa "Mkubwa" ili kumtofautisha na Mtume mwingine mwenye jina hilohilo, Yakobo Mdogo mwana wa Alfayo.
Yaliyomo |
Maisha ya awali [hariri]
Yakobo pamoja na baba na mdogo wake walikuwa wavuvi huko Kafarnaumu kwenye Ziwa la Galilaya.
Wataalamu kadhaa wanadhani walikuwa pia makuhani.
| Mitume wa Yesu |
|---|
|
Wito wa utume [hariri]
Inakadiriwa alikutana na Yesu mwaka 28.
Pamoja na mdogo wake waliitwa na Yesu Boanerghes ("wanangurumo") kutokana na umotomoto wao.
Pamoja na mitume wengine waliongozana na Yesu Kristo miaka mitatu hivi, ambapo Yakobo alionekana kuwa karibu sana na Yesu na kuchaguliwa naye kushuhudia matukio kadhaa ya pekee (ufufuo wa binti Yairo, kugeuka sura mlimani, kihoro bustanini).
Baada ya ufufuko wa Yesu [hariri]
Baada ya kifo na ufufuko wa Yesu, Yakobo alishika nafasi ya maana katika jumuia ya kwanza ya Wakristo wa Yerusalemu.
Mwaka 44 hivi aliuawa na Herode Agripa I kwa upanga (Matendo ya Mitume 12:1-2), wa kwanza kumfia Yesu kati ya Mitume wake.
Heshima yake [hariri]
Anaheshimiwa na Wakristo wote kama mtakatifu, hasa tarehe 25 Julai huko Santiago de Compostella (Hispania, ambapo wengi wanaamini aliwahi kufika kiutume).
Marejeo [hariri]
- Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1
Viungo vya nje [hariri]
- "St. James the Great, Apostle", Butler's Lives of the Saints
- The Life, Miracles and Martyrdom of St. James the Great: Apostle and Martyr of the Christian Church
- The Way of St. James Guide for the pilgrimage to Santiago de Compostela following St. James's footsteps.
- Catholic Encyclopedia: St James the Greater
- R. A. Fletcher, Saint James's Catapult: The Life and Times of Diego Gelmírez of Santiago de Compostela Oxford University Press, 1984: chapter 3, "The Early History of the Cult of St. James"
- Apostle James the Brother of St John the Theologian Orthodox icon and synaxarion
- History