Miujiza ya Yesu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kristo Akitembea juu ya Maji, kadiri ya Ivan Aivazovsky, 1888.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Miujiza ya Yesu ni matendo yapitayo sheria za maumbile[1] yaliyofanywa na Yesu kadiri yanavyosema maandiko matakatifu ya Ukristo na Uislamu. Ilikuwa mingi sana; hata hivyo Injili ya Yohane (21:25) inashuhudia kwamba michache tu imeandikwa.[2][3][4]

Kati ya miujiza hiyo, kuna mazinguo ya kufukuza pepo wachafu, uponyaji wa maradhi mbalimbali (homa, ukoma, safura, kupooza mkono au mwili mzima, kupinda kwa mgongo, kutokwa damu mfululizo, upofu, uziwi, ububu na vilema vingine), ufufuo wa wafu, na ushindi juu ya uasilia (kama kugeuza maji kuwa divai, kutembea juu ya maji ya ziwa, kutuliza dhoruba na kuzidisha mkate na kitoweo cha samaki).[5][6]

Ukweli wa kihistoria[hariri | hariri chanzo]

Kwa Wakristo na Waislamu, miujiza kama hiyo ilitokea kweli.[7]

Baadhi ya wataalamu wanatoa hoja ili kuthibitisha hilo.[8][9]

Kama kawaida, watu wengine wanakanusha dai hilo au wanasema miujiza ni mifano ya mambo ya kiroho tu.[10]

Maana yake[hariri | hariri chanzo]

Miujiza ilikuwa na umuhimu wake katika utume wa Yesu, ikishuhudia mamlaka yake ya Kimungu[3], kama vile njaa, kiu, uchovu na mateso vinavyoshuhudia ubinadamu wake.[11][12][13]

Pamoja na hayo, miujiza ilitokana pia na upendo na huruma yake kwa binadamu mwenye shida.[3][14]

Miujiza ililenga pia kutoa ujumbe kwa matendo ili kufafanua na kuthibitisha maneno kama vile haja ya kuwa na imani.[15][16] Kila muujiza ulikuwa na fundisho maalumu.

Miujiza inayosimuliwa nje ya Biblia[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vya kale (kuanzia karne ya 2) ambavyo havikukubalika katika Agano Jipya la Biblia ya Kikristo vinasimulia miujiza mingine ambayo Yesu aliweza kufanya tangu utotoni. Vitabu hivyo ni kama Injili ya Siri ya Marko 1, Injili ya Utoto ya Thoma 2.2, 2.3, 9-18, Injili ya Yakobo 19-20.

Picha za miujiza[hariri | hariri chanzo]

Sanaa ya Kikristo imechochewa na miujiza hiyo, kwa mfano katika michoro ifuatavyo.

Uponyaji[hariri | hariri chanzo]

Mazinguo[hariri | hariri chanzo]

Ufufuo[hariri | hariri chanzo]

Utawala juu ya maumbile[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Baker Theological Dictionary of the Bible defines a miracle as "an event in the external world brought about by the immediate agency or the simple volition of God." It goes on to add that a miracle occurs to show that the power behind it is not limited to the laws of matter or mind as it interrupts fixed natural laws. So the term supernatural applies quite accurately. Elwell, Walter A., ed. (2001). Baker Theological Dictionary of the Bible. Baker Academic. ISBN 978-0801022562 .
  2. Harris, Stephen L., Understanding the Bible. Palo Alto: Mayfield. 1985. "John" p. 302-310
  3. 3.0 3.1 3.2 Catholic Encyclopedia on Miracles
  4. The emergence of Christian theology by Eric Francis Osborn 1993 ISBN 0-521-43078-X page 100
  5. Graham H. Twelftree, Jesus the Miracle Worker: A Historical and Theological Study (InterVarsity Press, 1999) page 263.
  6. H. Van der Loos, 1965 The Miracles of Jesus, E.J. Brill Press, Netherlands.
  7. "Islamic beliefs include many miracles of healing and of resurrection of the dead." Heribert Busse, 1998 Islam, Judaism, and Christianity, ISBN 1-55876-144-6 page 114
  8. Graham H. Twelftree, Jesus the miracle worker: a historical & theological study ISBN 0-8308-1596-1 page 19
  9. Gary R. Habermas, 1996 The historical Jesus: ancient evidence for the life of Christ ISBN 0-89900-732-5 page 60
  10. Mark Allan Powell, Jesus as a Figure in History: How Modern Historians View the Man from Galilee (Westminster John Knox Press, 1998), page 22.
  11. Lockyer, Herbert, 1988 All the Miracles of the Bible ISBN 0-310-28101-6 page 25
  12. William Thomas Brande, George William Cox, A dictionary of science, literature, & art London, 1867, also Published by Old Classics on Kindle, 2009, page 655
  13. Bernard L. Ramm 1993 An Evangelical Christology ISBN 1-57383-008-9 page 45
  14. Author Ken Stocker states that "every single miracle was an act of love": Facts, Faith, and the FAQs by Ken Stocker, Jim Stocker 2006 ISBN page 139
  15. Berard L. Marthaler 2007 The creed: the apostolic faith in contemporary theology ISBN 0-89622-537-2 page 220
  16. Lockyer, Herbert, 1988 All the Miracles of the Bible ISBN 0-310-28101-6 page 235

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Miujiza ya Yesu kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.