Kiaramu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Herufi za kiaramu

Kiaramu ni mojawapo kati ya lugha za Kisemiti ambazo zinapangwa kati ya lugha za Afrika-Asia pamoja na Kiebrania na nyinginezo.

Inatumika tangu miaka 3,000 iliyopita. Ndiyo lugha aliyoitumia Yesu pamoja na Wayahudi wengi wa wakati wake.

Sehemu chache za Biblia ziliandikwa kwa lugha hiyo wakati ilipokuwa imeenea zaidi kwenye Mashariki ya Kati hata Kiaramu cha Kale kikawa lugha rasmi ya utawala katika Milki ya Uajemi.

Baada ya Aleksander Mkuu wasemaji wa Kiaramu walitawaliwa na watu wa ustaarabu wa Kigiriki. Katika miji mikubwa Kigiriki kilikuwa lugha kuu. Baada ya uenezaji wa Ukristo lugha hiyo iliendelea ikajulikana zaidi kama "Kisiria".

Hata baada ya uenezi wa Uislamu Kisiria kiliendelea kupanuka na vitabu vingi viliandikwa kwa lugha hiyo. Hata hivyo polepole wasemaji wengi wa Kisiria walianza kutumia Kiarabu, hasa wale waliogeukia Uislamu.

Pamoja na hayo watu 445,000 hivi wanaitumia hata leo, hasa nchini Syria, Iraq na Uturuki. Karibu wote ni Wakristo.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiaramu kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.