Kitigrinya
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kitigrinya (pia: Kitigray, Kitigre, Kihabesha) ni lugha ya Kisemiti inayozungumzwa katika Ethiopia (hasa jimbo la Tigray) na Eritrea.
Idadi ya wasemaji ni takriban milioni 5-6. Maandishi yake ni kwa alfabeti ya Kiethiopia. Kitigrinya kimetoka katika lugha ya kale ya Ge'ez iliyokuwa lugha ya nyanda za juu za Ethiopia na hadi leo ni lugha ya liturgia katika kanisa la Kiorthodoksi la Ethiopia na Eritrea.
Katika Ethiopia Kitigrinya ni lugha ya tatu inayotumiwa na watu wengi (baada ya Kioromo na Kiamhari). Katika Eritrea ni lugha inayotumiwa zaidi kabisa.
[hariri] Viungo vya nje
| Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kitigrinya kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |