Kiyoruba
Kiyoruba ni lugha ya Kiniger-Kongo hasa nchini Nigeria inayozungumzwa na Wayoruba. Ni lugha rasmi mojawapo ya nchi ya Nigeria. Mwaka wa 1993 idadi ya wasemaji wa Kiyoruba nchini Nigeria imehesabiwa kuwa watu karibu milioni 19. Pia kuna wasemaji 465,000 nchini Benin. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiyoruba kiko katika kundi la Kidefoidi.
Viungo vya nje[hariri]
- lugha ya Kiyoruba kwenye Multitree
- ramani ya Kiyoruba
- http://www.ethnologue.org/show_language.asp?code=yor
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.