Kizulu
Kizulu (isiZulu) ni lugha ya Wazulu inayoongelewa nchini Afrika Kusini, na idadi ya watu wanaokadiriwa kuwa milioni 9-10 hasa katika jimbo la KwaZulu-Natal. Kizulu huhesabiwa kati ya lugha za Kinguni ndani ya lugha za Kibantu.
Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kizulu nchini Afrika Kusini imehesabiwa kuwa watu 9,980,000. Pia kuna wasemaji nchini Botswana, Lesotho, Malawi, Msumbiji na Uswazi. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kizulu kiko katika kundi la S40.
Wakati wa mfecane katika karne ya 19 wasemaji wa lugha ya Kizulu zimehama hadi Zimbabwe, Zambia, Msumbiji na Tanzania ambako lugha imebadilika kiasi kuwa kwa mfano Kindebele au Kingoni.
Viungo vya nje [hariri]
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.