Kiwolofu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta

Kiwolofu ni lugha iongewayo nchini Senegal, Gambia, na Mauritania. Ni lugha rasmi kwa Wawolofu. Lugha hii ipo kama lugha jirani ya Fula inayohesabiwa kati ya lugha za Kiatlantiki cha familia ya lugha za Niger-Kongo.

Kiwolofu ni lugha inayoongelewa sana nchini Senegal, haizungumzwi na Wawolofu tu (karibuni asilia 40 ya watu huzungumza kama lugha ya mama) bali hata Wasenegal wengine huzumgumza lugha hii. Lahaja za Kiwolofu zaweza kufanana sana kati ya nchi hizi mbili, yaani Senegal na Gambia, zikiwa sambamba kabisa kitabia na hata kuongelewa kieneo.

Idadi ya wasemaji kama lugha ya mama ni takriban milioni 3.2 na karibu idadi ileile hutumia Kiwolofu kama lugha ya pili.

Kuna lahaja mbalimbali kama vile "Dakar-Wolof". Dakar ni mji wenye watu mchanganyiko, yaani kunawaongeaji wa Kiwolofu, Kifaransa, Kiarabu, na hata Kiingereza huzungumzwa kidogo pia katika mji huo wa Dakar, mji ambao uko nchini Senegal.

Viungo vya Nje [hariri]


Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.