Kiafrikaans

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Majimbo ya Afrika Kusini penye wasemaji wengi au wengi kidogo wa Kiafrikaans kama lugha ya kwanza

Kiafrikaans (Afrikaans) ni lugha ya Afrika Kusini iliyotokea katika karne nne zilizopita kwenye msingi wa Kiholanzi pamoja na athari za lugha mbalimbali. Imekuwa lugha rasmi katika Afrika Kusini tangu mwaka 1925 badala ya Kiholanzi. Hata kama ni lugha iliyozaliwa Afrika kitaalamu ni kati ya lugha za Kigermanik.

Kiafrikaans ina wasemaji wa lugha ya kwanza milioni sita na milioni kumi wasemaji kama lugha ya pili.

Kiasili kimetokea kama lugha ya makaburu ya Afrika Kusini lakini imekuwa pia lugha ya wakazi chotara katika jimbo la Rasi Magharibi ("Cape Coloureds"). Leo hii wasemaji wa asili ya Ulaya ni chini ya nusu ya wasemaji wote wa Kiafrikaans.

Ni lugha rasmi mojawapo Afrika Kusini pamoja na lugha 9 nyingine. Ni pia kati ya lugha ya kitaifa huko Namibia.

Viungo vya nje [hariri]


Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.