Maeneo ya Kihistoria ya Kitaifa ya Tanzania
Maeneo ya Kihistoria ya Kitaifa ya Tanzania ni orodha kuu rasmi ya maeneo mbalimbali nchini Tanzania ambayo yameteuliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii ya Tanzania chini katika Kitengo cha Mambo ya Kale. [1] Orodha hii haijakamilika na inafanyiwa kazi kwa sasa.
Historia[hariri | hariri chanzo]
Historia ya Idara ya Mambo ya Kale na Maeneo ya Kihistoria ya Kitaifa iliundwa na mamlaka ya Waingereza katika eneo la Tanganyika mwaka 1937 kama Sheria ya Uhifadhi wa Maziara ya mwaka wa 1937. Ilipofika mwaka wa 1957, idara hiyo ilikabidhiwa kwa Wizara ya Elimu kama Kitengo cha Mambo ya Kale kilichozinduliwa na ofisi iliyopo Bagamoyo, mkoa wa Pwani. Ofisi ilihamishiwa rasmi kwenda Dar es Salaam mwaka 1960. Ulipofikia mwaka wa 1964, miaka mitatu baada ya uhuru wa taifa, Bunge la taifa la Tanzania lilipitisha Sheria ya Mambo ya Kale Na. 10 ya mwaka 1964 ili kuchukua nafasi ya Sheria ya Uhifadhi wa Makumbusho ya 1937. [2] Sheria ya 1964 ilirekebishwa mwaka wa 1979 na kuwekwa kwa Sheria ya Mambo ya Kale Na. 22 ya mwaka 1979, kisha hiyo nayo ikabadilishwa na Sheria ya Makumbusho ya Vitu Na. 13 ya mwaka 1981 ambao ndiyo sheria iliyomo mpaka leo. [3]
Orodha ya Maeneo ya Kihistoria ya Kitaifa[hariri | hariri chanzo]
Ifuatayo hapo chini ni orodha ya Maeneo ya Kihistoria ya Kitaifa ya nchi ya Tanzania. [4] Kuna tovuti za ziada kwa mikoa kwenye hii orodha. [5]
Mkoa wa Tanga[hariri | hariri chanzo]
- Magofu ya Tongoni (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Mapango ya Amboni
- Lushoto (Makazi ya Zama za Chuma)
- Kisiwa cha Toten (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Pangani (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
Mkoa wa Arusha[hariri | hariri chanzo]
- Olduvai Gorge (Mabaki ya zamadamu)
- Laetoli (Mabaki ya zamadamu)
- Mifereji ya Umwagiliaji Engaruka
- Nasera Rockshelter (Makazi ya Zama za Mawe)
- Pango la Mumba (Zama za Mawe na Zama za Chuma)
Mkoa wa Manyara[hariri | hariri chanzo]
- Luxmanda (Zama Mpya za Mawe)
Mkoa wa Kilimanjaro[hariri | hariri chanzo]
- Pare (Makazi ya Zama za Chuma)
- Bombo Kaburi (Makazi ya Zama za Chuma)
- Usangi (Makazi ya Zama za Chuma)
Mkoa wa Manyara[hariri | hariri chanzo]
- Naberera (Kazi za Mazishi)
Mkoa wa Pwani[hariri | hariri chanzo]
- Mji wa kihistoria wa Bagamoyo
- Magofu ya Kaole (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Chole (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Kisimani Malia (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Kisiju (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Mkiu (Makazi ya Zama za Chuma)
Mkoa wa Morogoro[hariri | hariri chanzo]
- Dakawa (Makazi ya Zama za Chuma)
- Milima ya Ngulu (Makazi ya Zama za Chuma)
Mkoa wa Dodoma[hariri | hariri chanzo]
- Michoro ya miambani ya Kondoa Irangi
- Lelesu (Makazi ya Zama za Chuma)
- Michoro ya miambani ya Bahi
Mkoa wa Tabora[hariri | hariri chanzo]
Mkoa wa Mwanza[hariri | hariri chanzo]
Mkoa wa Kigoma[hariri | hariri chanzo]
- Makumbusho ya Livingstone ya Ujiji
- Uvinza (Makazi ya Zama za Chuma)
Mkoa wa Mbeya[hariri | hariri chanzo]
- Kimondo cha Mbozi
- Maporomoko ya Kala (Makazi ya Zama za Mawe)
- Ivuna (Makazi ya Zama za Chuma)
Mkoa wa Songwe[hariri | hariri chanzo]
- Maporomoko ya Kalambo (Makazi ya Zama za Mawe na ya Zama za Chuma)
Mkoa wa Rukwa[hariri | hariri chanzo]
Mkoa wa Iringa[hariri | hariri chanzo]
Mkoa wa Lindi[hariri | hariri chanzo]
- Kilwa Kisiwani (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Kilwa Kivinje (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Magofu ya Songo Mnara (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Sanje ya Kati (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Tendaguru (Makazi ya Zama za Mawe)
Mkoa wa Mtwara[hariri | hariri chanzo]
- Mji wa kihistoria wa Mikindani
Mkoa wa Ruvuma[hariri | hariri chanzo]
Mkoa wa Kagera[hariri | hariri chanzo]
- Makumbusho ya Bweranyange
- Kemondo KM2 na KM3 (Makazi ya Zama za Chuma)
- Katuruka (Makazi ya Zama za Chuma)
- Kansyore (Makazi ya Zama za Chuma)
- Nyabusora (Makazi ya Zama za Mawe)
Mkoa wa Dar es Salaam[hariri | hariri chanzo]
- Magofu ya Kunduchi (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Magomeni Makumbusho
- Mbweni (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Msasani (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
Mkoa wa Unguja Kaskazini[hariri | hariri chanzo]
- Tumbatu ((Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi[hariri | hariri chanzo]
- Mji Mkongwe (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
Mkoa wa Unguja Kusini[hariri | hariri chanzo]
- Unguja Ukuu (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Pango la Kuumbi
Mkoa wa Pemba Kusini[hariri | hariri chanzo]
- Chake Chake (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Pujini (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
- Maghofu ya Ras Mkumbuu (Makazi ya Waswahili wa Zama za Kati)
Uongozi na Wizara[hariri | hariri chanzo]
Ifuatayo ni historia ya idara ya mambo ya kale nchini Tanzania; imekuwa chini ya uongozi wa watu wafuatao: [6]
*1957-1968: Neville Chittick, Mtunza
*1968-1981: Amin Aza Mutri, Mkurugenzi
*1981-1985: Simon S.A. Waane, Mkuu wa Sehemu
*1985-1997: Simon SA Waane, Mkurugenzi
*1997-2000: Donatius M.K. Kamamba, Ag Mkurugenzi
*2000-Hadi sasa: Donantius M.K. Kamamba, Mkurugenzi
Idara ya Mambo ya Kale ya Tanzania imekuwa chini ya wizara zifuatazo:
*1957-1962: Wizara ya Elimu
*1962-1964: Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana
*1964-1967: Ofisi ya Rais 1967-1968: Wizara ya Tawala za Mikoa *1968-1980: Wizara ya Elimu ya Taifa
*1980 -1984: Wizara ya Habari na Utamaduni
*1984-1999: Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Utamaduni, Vijana na Michezo
*1999–Sasa: Wizara ya Maliasili na Utalii.
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ https://www.maliasili.go.tz/sectors/category/antiquities
- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-11-03. Iliwekwa mnamo 2021-12-22.
- ↑ http://www.parliament.go.tz/polis/uploads/bills/acts/1566374555-The%20Antiquities%20(Amendment)%20Act,%201979.pdf
- ↑ https://www.maliasili.go.tz/uploads/ANTIQUITIES_SITES_LOCATION_AND_ACCESSBILITY.pdf
- ↑ https://www.nps.gov/CRMJournal/winter2010/article1.html
- ↑ https://www.maliasili.go.tz/sectors/category/antiquities