Paulo Miki
Mandhari

Paulo Miki (Kyoto, takriban 1565 – Nagasaki, 5 Februari 1597) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki nchini Japani.
Ametambuliwa kuwa mtakatifu kama mfiadini.
Sikukuu yake ni tarehe 6 Februari[1].
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Paulo Miki alizaliwa nchini Japani kati ya miaka 1564 na 1566.
Alijiunga na Shirika la Yesu (Wajesuiti), akahubiri Injili kwa ufanisi [2].
Lakini dhuluma dhidi ya Wakatoliki zilipozidi, yeye na wenzake 25 (mapadri na watawa 8 na walei 17[3]) walikamatwa, walitukanwa na kuteswa vikali, na hatimaye wakasulubiwa huko Nagasaki tarehe 5 Februari mwaka 1597, huku wakifurahia neema ya kuuawa namna ileile ya Yesu [4].
Hadi sasa Wafiadini wa Japani waliotangazwa watakatifu ni 42, mbali na wenye heri 393.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/22700
- ↑ Kati yao Yohane wa Goto na Yakobo Kisai walikuwa Wajesuiti; Petro Baptista, Martino wa Kupaa na Fransisko Blanco, walikuwa mapadri wa shirika la Ndugu Wadogo Pekupeku; Filipo wa Yesu, Gonzalo Garcia na Fransisko wa Mt. Mikaeli walikuwa mabradha wa shirika hilohilo; Leo Karasuma, Petro Sukejiro, Kosma Takeya, Paulo Ibaraki, Tomaso Danki, Paulo Suzuki walikuwa makatekista Wajapani; Ludoviko Ibaraki, Antoni wa Nagasaki, Mikaeli Kozaki na mwanae Tomaso, Bonaventura, Gabrieli, Yohane Kinuya, Matia, Fransisko wa Meako, Yohakimu Sakakibara na Fransisko Adaukto walikuwa Wakristo wapya.
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/93366
Marejeo ya Kiswahili
[hariri | hariri chanzo]- Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 54-57
- Sala ya Kanisa ya Ki-fransisko - Benedictine Publications Ndanda - Peramiho, 1996, uk 36-40
- John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 47
- Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 426-428
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |