Paulinus wa York
Paulinus wa York (alifariki 10 Oktoba 644) alikuwa mmisionari kutoka Roma nchini Uingereza aliyefanywa askofu wa kwanza wa York[1].
Maisha[hariri | hariri chanzo]
Akiwa kati ya wamonaki waliotumwa na Papa Gregori I ili kuinjilisha Waangli na Wasaksoni, Paulinus alifika mwaka 604 katika kundi la pili.
Baada ya kuishi miaka huko Kent, tarehe 21 Julai 625 alipewa daraja takatifu ya uaskofu. Aliposindikiza Æthelburg wa Kent kwenda Northumbria kuolewa na Edwin wa Northumbria, alifaulu kumuongoa Edwin kuingia Ukristo pamoja na raia wake wengi. Kati yao alikuwepo Hilda wa Whitby. Pia alijenga makanisa kadhaa.
Edwin alipofariki (633), Paulinus na Æthelburg walikimbia Northumbria, wakimuacha nyuma James Shemasi. Huko Kent, Paulinus akawa askofu wa Rochester akapokea paliumu kutoka kwa Papa, ikiwa na maana ya kufanywa askofu mkuu wa York, ingawa hakupata nafasi ya kwenda[2].
Tangu kale Paulinus anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ http://www.santiebeati.it/dettaglio/92490
- ↑ Lapidge "Ecgbert" Blackwell Encyclopedia of Anglo-Saxon England
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- Blair, Peter Hunter (1990). The World of Bede (toleo la Reprint of 1970). Cambridge, UK: Cambridge University Press. ISBN 0-521-39819-3.
- Costambeys, Marios (2004). "Paulinus (St Paulinus) (d. 644)". Oxford Dictionary of National Biography (October 2005 revised ed.). Oxford University Press.
. http://www.oxforddnb.com/view/article/21626. Retrieved 6 March 2009.
- Farmer, David Hugh (2004). Oxford Dictionary of Saints (toleo la Fifth). Oxford, UK: Oxford University Press. ISBN 978-0-19-860949-0.
- Fryde, E. B.; Greenway, D. E.; Porter, S.; Roy, I. (1996). Handbook of British Chronology (toleo la Third revised). Cambridge, UK: Cambridge University Press. ISBN 0-521-56350-X.
- Kirby, D. P. (2000). The Earliest English Kings. New York: Routledge. ISBN 0-415-24211-8.
- Lapidge, Michael (2001). "Ecgberht". The Blackwell Encyclopaedia of Anglo-Saxon England. Malden, MA: Blackwell Publishing. p. 157.
.
- Lapidge, Michael (2001). "Paulinus". The Blackwell Encyclopaedia of Anglo-Saxon England. Malden, MA: Blackwell Publishing. p. 359.
.
- Mayr-Harting, Henry (1991). The Coming of Christianity to Anglo-Saxon England. University Park, PA: Pennsylvania State University Press. ISBN 0-271-00769-9.
- Rollason, David. "The shrines of saints in later Anglo-Saxon England: Distribution and significance" (pdf). Archaeology Data Services. Department of Archaeology, University of York. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 13 June 2011. Iliwekwa mnamo 29 March 2009. Check date values in:
|archivedate=, |accessdate=
(help) - Sharpe, R. (September 2002). "The Naming of Bishop Ithamar". The English Historical Review 117 (473): 889–894. JSTOR 3489611. doi:10.1093/ehr/117.473.889. Check date values in:
|date=
(help) - Stenton, F. M. (1971). Anglo-Saxon England (toleo la Third). Oxford, UK: Oxford University Press. ISBN 978-0-19-280139-5.
- Walsh, Michael J. (2007). A New Dictionary of Saints: East and West. London: Burns & Oats. ISBN 0-86012-438-X.
- Williams, Ann (1999). Kingship and Government in Pre-Conquest England c. 500–1066. London: MacMillan Press. ISBN 0-333-56797-8.
- Yorke, Barbara (2006). The Conversion of Britain: Religion, Politics and Society in Britain c. 600–800. London: Pearson/Longman. ISBN 0-582-77292-3.
- Yorke, Barbara (1997). Kings and Kingdoms of Early Anglo-Saxon England. New York: Routledge. ISBN 0-415-16639-X.
Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]
- Mayr-Harting, H. M. R. E. (1967). "Paulinus of York". In G. J. Cuming. Studies in Church History IV: The Province of York. Leiden: Brill. pp. 15–21.
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |