Askofu mkuu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Askofu mkuu ni cheo cha askofu kiongozi anayesimamia maaskofu katika jimbo la kanisa lenye dayosisi mbalimbali.

Asili ya neno lenyewe ni Kigiriki αρχή arché (mwanzo, wa kwanza). Sehemu ya pili ni neno la Kigiriki επίσκοπος episkopos (mwangalizi) lililofikia Kiswahili kupitia umbo la Kiarabu uskuf.

Kanisa katoliki[hariri | hariri chanzo]

Kama nchi ina wakatoliki wengi kuna majimbo mbalimbali na kila moja ina askofu mkuu wake. Kama idadi ya wakatoliki ni wastani huwa na jimbo moja na askofu mmoja tu mwenye cheo cha askofu mkuu.

Waanglikana na Waluteri[hariri | hariri chanzo]

Katika makanisa mengine huwa askofu mkuu ni askofu kiongozi wa nchi fulani. Lakini cheo hiki hakitumiwi vile katika kila nchi na Waluteri ni hasa Waluteri wa Uswidi, Ufini, Urusi na Estonia walio na askofu mkuu.

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Askofu mkuu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.